Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan azungumza na Wananchi wa Laela Mkoani Rukwa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Laela mara baada ya kuweka jiwe la Msingi la ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Rukwa tarehe 17 Julai, 2024

Shamrashamra za Wananchi wa Laela wakati wakimpokea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika muendelezo wa Ziara yake ya Kikazi Mkoani Rukwa tarehe 17 Julai, 2024.
 

Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aweka Jiwe la Msingi Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Rukwa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Rukwa mara baada ya kuweka jiwe la Msingi la ujenzi wa Shule hiyo kwenye hafla iliyofanyika katika Kijiji cha Mtindilo Laela mkoani humo tarehe 17 Julai, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuweka jiwe la Msingi la ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Rukwa kwenye hafla iliyofanyika katika Kijiji cha Mtindilo Laela mkoani humo tarehe 17 Julai, 2024.

Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan afungua jengo la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. DktSamia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria ufunguzi wa jengo la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo tarehe 16 Julai, 2024. Mhe. Rais Dkt. Samia anaendelea na Ziara yake ya kikazi Mkoani Rukwa ambapo pamoja na mambo mengine atazindua miradi ya maendeleo pamoja na kuzungumza na Wananchi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. DktSamia Suluhu Hassan akikata utepe kama ishara ya kufungua jengo la Utawala Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo tarehe 16 Julai, 2024. Mhe. Rais Dkt. Samia anaendelea na Ziara yake ya kikazi Mkoani Rukwa ambapo pamoja na mambo mengine atazindua miradi ya maendeleo pamoja na kuzungumza na Wananchi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. DktSamia Suluhu Hassan akipokea Taarifa ya Ujenzi wa jengo la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kutoka kwa Waziri wa TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa kabla ya ufunguzi tarehe 16 Julai, 2024.
Taswira ya Jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo ambalo limefunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. DktSamia Suluhu Hassan, tarehe 16 Julai, 2024. 

 




Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan afungua Barabara ya Sumbawanga, Matai-Kasanga (km107) Mkoani Rukwa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria ufunguzi wa barabara ya Sumbawanga-Matai-Kasanga (km107) iliyojengwa kwa kiwango cha lami. Hafla ya ufunguzi wa barabara hiyo imefanyika katika eneo la Matai Wilayani Kalambo Mkoani Rukwa tarehe 16 Julai, 2024.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria ufunguzi wa barabara ya Sumbawanga-Matai-Kasanga (km107) iliyojengwa kwa kiwango cha lami. Hafla ya ufunguzi wa barabara hiyo imefanyika Matai Wilayani Kalambo Mkoani Rukwa tarehe 16 Julai, 2024.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Matai katika Wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa mara baada ya kufungua barabara ya Sumbawanga-Matai-Kasanga (km107), tarehe 16 Julai, 2024.

Wananchi wa Matai, Kalambo Mkoani Rukwa wakiwa kwenye mkutano wa hadhara pamoja na hafla ya ufunguzi wa Barabara ya Sumbawanga-Matai-Kasanga (km107) iliyojengwa na kukamilika kwa kiwango cha lami katika eneo la Matai tarehe 16 Julai, 2024.


Taswira ya Barabara ya Sumbawanga-Matai-Kasanga (km107) iliyojengwa na kukamilika kwa kiwango cha lami

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akikagua Barabara ya Sumbawanga-Matai-Kasanga (km107) iliyojengwa na kukamilika kwa kiwango cha lami katika eneo la Matai tarehe 16 Julai, 2024.




Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aweka jiwe la Msingi upanuzi na ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga Mkoani Rukwa


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa kuashiria uzinduzi vihenge na maghala ya kisasa ya kuhifadhia nafaka ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi wa Chakula (NFRA), Kanondo, Sumbawanga Mkoani Rukwa tarehe 16 Julai, 2024. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akibonyeza kitufe kuashiria ununuzi wa nafaka kwa msimu wa 2024-2025 mara baada ya uzinduzi wa vihenge na maghala ya kisasa ya kuhifadhia Nafaka ya (NFRA), Kanondo, Sumbawanga Mkoani Rukwa katika muendelezo wa Ziara yake ya Kikazi mkoani rukwa tarehe 16 Julai, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi mara baada ya kuzindua vihenge na maghala ya kisasa ya kuhifadhia nafaka ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi wa Chakula (NFRA) Kanondo, Sumbawanga Mkoani Rukwa tarehe 16 Julai, 2024. 
Vihenge na maghala ya kisasa ya kuhifadhia nafaka ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi wa Chakula (NFRA) yaliyopo Kanondo, Sumbawanga Mkoani Rukwa tarehe 16 Julai, 2024. 
Muonekano wa Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga ambacho ambacho kipo kwenye hatua mbalimbali za ujenzi kama inavyoonekana. 


Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aanza Ziara ya Kikazi Mkoani Rukwa kwa kuzindua Hospitali ya Wilaya ya Nkasi iliyopo Namanyere


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Namanyere mara baada ya kuzindua Hospitali ya Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa tarehe 15 Julai, 2024. Mhe. Rais Dkt. Samia ameanza Ziara yake ya kikazi Mkoani Rukwa ambapo pamoja na mambo mengine atazindua miradi ya maendeleo pamoja na kuzungumza na Wananchi.

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa