MADINI YOTE NCHINI NI SHARTI YA WANUFAISHE WATANZANIA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Naibu Waziri wa Madini nchini Mhe Doto Mashaka Biteko akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mkomola 2, Kata ya Kipande, Wilayani Nkasi akiwa katika ziara ya kikzai Mkoani Rukwa, Leo 23 Februari 2018. Picha Zote Na Mathias Canal-Wazo Huru Blog
Mhandisi Joseph Mwakabage Meneja Mradi wa Mradi wa uzalishaji wa umeme wa makaa ya mawe (Aliyenyoosha mkono) akimuonyeshaNaibu Waziri wa Madini nchini Mhe Doto Mashaka Biteko mitambo ya uchimbaji madini  alipotembelea mgodi huo uliopo Kijiji cha Mkomola 2, Kata ya Kipande, Wilayani Nkasi akiwa katika ziara ya kikzai Mkoani Rukwa, Leo 23 Februari 2018.
Naibu Waziri wa Madini nchini Mhe Doto Mashaka Biteko akikagua eneo la uchimbaji madini ya makaa ya mawe alipotembelea mgodi wa Edenville Tanzania Ltd uliopo Kijiji cha Mkomola 2, Kata ya Kipande, Wilayani Nkasi akiwa katika ziara ya kikzai Mkoani Rukwa, Leo 23 Februari 2018.
Mhandisi Joseph Mwakabage Meneja Mradi wa Mradi wa uzalishaji wa umeme wa makaa ya mawe (Kulia) akimueleza Naibu Waziri wa Madini nchini Mhe Doto Mashaka Biteko juu ya uchimbaji wa makaa ya mawe alipotembelea mgodi huo uliopo Kijiji cha Mkomola 2, Kata ya Kipande, Wilayani Nkasi akiwa katika ziara ya kikzai Mkoani Rukwa, Leo 23 Februari 2018.

Na Mathias Canal, Rukwa

Serikali imesema kuwa sheria mpya ya Madini ya mwaka 2010 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2017 inaelekeza wazi kuwa Madini yote nchini ni Mali ya watanzania hivyo wanapaswa kutambua umuhimu wa rasilimali.

Wawekezaji na wachimbaji wote wa madini nchini wanapaswa kutambua kuwa wanalo jukumu muhimu la kurejesha kwa jamii asilimia chache ya kile wanachozalisha kwa kuunga mkono juhudi za serikali Back to the Community) katika kuboresha miundombinu, sekta ya elimu, afya N.K

Naibu Waziri wa Madini nchini Mhe Doto Mashaka Biteko amesisitiza hayo Leo 23 Februari 2018 wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mkomola 2, Kata ya Kipande, Wilayani Nkasi wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la mradi wa uzalishaji wa umeme wa makaa ya mawe Mkoani Rukwa Magharibi mwa Tanzania.

Mradi huo unaosimamiwa na kampuni ya Edenville Tanzania Ltd kwa ubia na kampuni ya Edenville Energy of Uk na Upendo Group (Kampuni ya kizawa) ilianza shughuli za majaribio ya uchimbaji na uoshaji mwezi wa kumi mwaka Jana 2017 na mkaa wa kwanza kuuzwa kwa majaribio ni mwezi Novemba mwaka 2017.

"Nataka niwajulishe tu watanzania wenzangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli aliniteua kusimamia Wizara ya Madini nikimsaidia Waziri wetu Mhe Anjelina Kairuki ili kuboresha sekta hii ya Madini hatimaye kuwanufaisha watanzania kuliko ilivyokuwa awali ambapo Madini yalikuwa yanachimbwa nchini lakini faida inaenda nchi zingine" Alisema Mhe Biteko na Kuongeza kuwa

Wawekezaji hao wanapaswa kutoa ajira zisizo za utaalamu kwa wananchi wanaozunguka migodi yao sambamba na watanzania wote huku akiwaagiza kuwaajiri wataalamu wa Madini wa ndani ya nchi kwa kazi ambazo wanaweza kuzifanya sio kuajiri wageni.

Aidha, aliwasisitiza wananchi hao pindi wanapopata ajira zao katika migodi mbalimbali wanapaswa kuwa waaminifu ili kuwavutia wawekezaji hao jambo litakalopelekea wawekezaji kuwa na imani na watanzania na hatimaye kuongeza chachu ya ajira nyingi zaidi.

Sambamba na hayo amekemea baadhi ya wafanyakazi katika migodi mbalimbali ambao wameaminiwa na kupatiwa ajira lakini wanageuza muda wa kazi kuwa muda wa starehe kwa kunywa pombe na utoro kazini.

Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko yupo katika ziara ya kikazi ya siku mbili Mkoani Rukwa kutembelea na kukagua uchimbaji wa Madini.

Tatu Mzuka yazidi kuwaneemesha Watanzania,wengi waendelea kujizolea mamilioni

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Mwakilishi wa Kampuni ya inayochezesha mchezo wa kubahatisha,TatuMzuka,Kemilembe Mbeikya (katikati),akizungumza mbele ya Wanahabari mapema jana wakati wa kuwatambulisha washindi wa TatuMzuka,ambao kulia ni Abraham Kisiri kutoka Mkwajuni Kinondoni aliyejishindia million 60 pamoja na Ummy Abraham kutoka Wazo hill, Tegeta alijishindia million 5.
Kemi alisema kuwa Tatu Mzuka jackpot ya wiki iliyopita imetoa jumla million 80 kwa washindi wa nne,wakiwemo wawili pichani na wengine ni Mathew Mtoni kutoka Songea aliyejishindia milioni 10 pamoja na Selemani Mkoko kutoka Nachingwea aliejishindia millioni 5.

Tatu Mzuka hadi leo imetoa billion 14 na kutengenza washindi million 6. Hawa washindi ni thibisho tosha kuwa Tatu Mzuka inabadilisha maisha ya watu.Kama unavyojua, Tatu Mzuka inakupa nafasi ya kushinda kila lisaa hadi million 6, na sasa hivi kwenye msimu wa Valentine, wewe na mpendanao mnaweza kushinda million kumi kila silku na bado una nafasi ya kushinda million 60 jumapili hii.
Ummy Abraham amabae ni wa Wazo hill, Tegeta jijini Dar Es Salaama akieleza namna alivyojishindia kitita cha shilingi million 5.Amesema kwa sasa fedha hizo zitamsaidia kuendelea kumsadia katika Matibabu ya Mumewe ambaye ni mgonjwa na pia Fedha nyingine amepanga kumaliza ukarabati wa nyumba zake mbili ili ziendelee kumuingizia kipato.Aidha Ummy ameishukuru TatuMzuka kwa kuleta mchezo ambao kwake umekuwa kama mkombozi kwa wakati aliokuwa nao kwa sasa.
Abraham Kisiri kutoka Mkwajuni Kinondoni jijini Dar,ambaye ni Dereva wa taasisi ya UVCCM alijishindia milioni 60.Abraham ameishukuru Tatu Mzuka kwa kuuleta mchezo huo kwa Wananchi,kwani umekuwa na manufaa makubwa kwa baadhi yao kiasi hata ya kuyabadilisha maisha yao,anasema kwa sasa fedha hizo atazitumia kujiimarisha zaidi kiuchumi .
Mwakilishi wa Kampuni ya inayochezesha mchezo wa kubahatisha,TatuMzuka,Kemilembe Mbeikya (katikati),akiwa na Washindi wa washindi wa TatuMzuka,ambao kulia ni Abraham Kisiri kutoka Mkwajuni Kinondoni aliyejishindia million 60 pamoja na Ummy Abraham kutoka Wazo hill, Tegeta alijishindia million 5 wakiwa sambamba na mfano wa hundi zao.

Wote waliolima,kuchoma mkaa msitu malangali wakamatwe maramoja-RC Wangabo

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akitoa agizo la kukamatwa kwa waliokiuka amri ya mahakama na kufanya shughuli za kibinadamu kwenye msitu wa Malangali Mjini Sumbawanga
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akitoa agizo la kukamatwa kwa waliokiuka amri ya mahakama na kufanya shughuli za kibinadamu kwenye msitu wa Malangali Mjini Sumbawanga katika Mkutano wa hadhara.


Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga Hamid Njovu akiwasilisha taarifa ya msitu wa Malangali uliopo Sumbawanga Mjini Kwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo.


Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ameagiza kuwasaka na kuwakamata wananchi wote waliokiuka amri ya mahakama ya kutoutumia msitu wa hifadhi ya Malangali kwaajili ya matumizi ya kibinadamu.

Amesema kuwa pamoja na kukamtwa, wananchi hao wasimamiwe kuhakikisha kuwa wanapanda miti maeneo ambayo wameyaharibu na kusisitiza kusakwa kwa wale wote waaofanya shughuli za kibinadamu kando ya vyanzo vya maji huku akitaja bonde la mto lwiche.

“Mpite shamba kwa shamba, kamateni watu wote ambao wamevamia kule, ule msitu uache kama ulivyo, vyanzo vyetu vya maji vitakauka, Mkurugenzi fanya msako wa bonde lote hilo kwa wale wote ambao wameanza kufyeka na kulima, kamata. DC simamia hili, tunataka kukomesha uharibifu wa mazingira wa aina yoyote ile,” Alisisitiza.

Ametoa agizo hilo katika mkutano wa hadhara alioufanya baada ya kutembelea msitu huo wa malangali uliopo kata ya Malangali, Wlayani Sumbawanga na kujione namna wananchi hao walivyoharibu msitu huo uliojaa miti ya miombo ambayo inakatwa na kugeuzwa mkaa.

Msitu huo wa Malangali ulianzishwa rasmi mwaka 1986 na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa huo Mh. Tumainieli Kihwelu wenye eneo la ekari 278 kwa lengo la kupunguza mmomonyoko na vimbunga.

Wakati akisoma taarifa ya Msitu huo Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbwanga Hamid Njovu amesema kuwa baada ya miaka 29 wananchi waliwasilisha malalamiko ya kupokonywa ardhi na kufanywa msitu shauri lililofikishwa mahakamani na kuamuliwa wananchi hao kulipwa fidia huku hukumu ya kesi hiyo ikisitisha shughuli zote za kibinadamu kutofanyika katika msitu huo.

“Tarehe 28/4/2016 hukumu ilitolea na kuamuliwa Manispaa ya Sumbawanga kulipa fidia huku Hukumu hiyo ikisitisha shughuli zote za kibinadamu ndani ya msitu lakini bado wananchi hao walirudi kufyeka miti na kulima na tarehe 13/11/2017 Manispaa ilitoa maelekezo kwa wananchi kutoutumia msitu kwa shughuli za kibinadamu,”Alimalizia. Mmoja wa wadau wa Mazingira Mzee Zeno Nkoswe amesema kuwa usalama wa mji wa Malangali unatokana na msitu huo na kwamba endapo utaendelea kuharibiwa mji huo utafunikwa na mmomonyoko wa udongo.

RC Wangabo awaibaini wakwepa kodi, atoa siku 7 wajirekebishe kabla ya Msako.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Mkuu wa MKoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo katika Baraza la Biashara la Mkoa akiwa na katibu Tawala wa Mkoa Benard Makali (wa kwanza kushoto) pamoja na Wenyeviti wa Halmashauri za Kalambo na Nkasi (Kulia)

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim wangabo amesikitishwa na kitendo cha wafanyabiashara kutumia mbinu mbalimbali za kukwepa kulipa kodi serikalini jambo linalorudisha nyuma maendeleo, hivyo kutoa siku saba za kujirekebisha kabla ya Mamlaka ya mapato kuanza msako mkali na kuwatia nguvuni.

Amesema kuwa katika kipindi cha mitatu kuanzia Oktoba hadi Disemba, 2017 Mamlaka ya Mapato Rukwa imekusanya shilingi bilioni 2.2 kiasi ambacho hakiendani na uhalisia na kuongeza kuwa Mamlaka hiyo inaweza kufanya vizuri zaidi endapo itapambana na vipingamizi vilivyopo.

“Kuna vipingamizi kadhaa moja ni wafanyabiashara kutokuwa na EFD, pili, baadhi ya wafanyabiashara kutotoa risiti, kuna wenye EFD mbili, iliyosajiliwa na isiyosajiliwa, na wao hutumia isiyosajiliwa na wengine kuwa na vitabu viwili vya stakabadhi na kutumia kile chenye mapato madogo kupiga mahesabu ya serikali, yote hii ni mianya ya kukwepa kodi ya serikali,na wengine kuuza kwenye magari bila ya risiti,” Alisisitiza.

Pia amebainisha kuwa kuna wafanyabiashara 316 ambao wamelipia mashine za EFD lakini hadi leo hawajapewa mashine hizo na kusababisha kuvuja kwa mapato ya serikali, ameyasema hayo katika mkutano wa Baraza la Biashara la Mkoa.

Katika kubainisha changamoto za wafanyabiashara mkoani humo Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara ,Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) Mkoa wa Rukwa Sadrick Malila amesema kuwa wafanayabiashara mkoani humo wamekuwa na wakati mgumu kutokana na utitiri wa kodi na kutokuwa na mahusiano mazuri na Mamlaka ya mapato Tanzania na kushauri kurudishwa kwa Jukwaa la walipa Kodi kwani lilikuwa na manufaa.

“Tulikuwa na jukwaa la walipa kodi, amabapo tulikuwa tunakaa na kujadili, lakini hili jukwaa limefutwa na kutoka pale imekuwa ubabe na wakati ule TRA walikuwa wanavuka malengo kuliko hali ilivyo hivi sasa,ambapo hawavuki malengo”Alisema

Tuhuma hizo zilikanushwa na Meneja wa Mamlaka ya Mapato TRA Mkoani Rukwa Fredrick Nyariri nae kutoa takwimu zilizobainisha kuvuka kwa malengo kulingana na viwango walivyopangiwa.

“Si kweli kwamba hatuvuki malengo kwa mfano mwezi Novembea tulipangiwa Shilingi Milioni 801 tukapata Milioni 928 na Mwezi Disemba tulipangiwa kukusanya Shilingi Milioni 908 na tukapata Milioni 996, nasikitika kusema kwamba taarifa ya mwenyekiti TCCIA imejaa upotoshaji,” Alimalizia. Na kuongeza kuwa Mamlaka ya Mapato imejipanga kuuza mashine za EFD na kuepukana na kuwa na wakala mmoja wa kusambaza mashine hizo ndani ya Mkoa wa Rukwa.

WANANCHI WAZIDI KUJIZOLEA MAMILIONI YA TATUMZUKA,WAZIDI KUNG'ARISHA MAISHA YAO.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


 

Meneja Mawasiliano kampuni ya michezo ya kubahatisha ya TatuMzuka,Sebastian Maganga akizungumza mbele ya Wanahabari (hawapo pichani,mapema jana jijini Dar wakati wa kuwatambulisha washindi wawili wa Tatumzuka waliopatikana mwishoni mwa wiki Jumapili Januari 21 2018, kupitia Mzuka Jackpot ambayo pia ilirushwa moja kwa moja kupitia vituo vya ITV, Clouds TV na TV1.Pichani kulia ni Mzee Emmanual Shayo kutoka Pugu Dar es Salaam ambaye alijishindia milioni 27. na kushoto ni Britony Mtalemwa kutoka Songea,ambaye alijishindia milioni 40.
Meneja Mawasiliano kampuni ya michezo ya kubahatisha ya TatuMzuka,Sebastian Maganga akimkabidhi mfano wa hundi Ndugu Britony Mtalemwa kutoka Songea,ambaye alijishindia milioni 40.
Meneja Mawasiliano kampuni ya michezo ya kubahatisha ya TatuMzuka,Sebastian Maganga akimkabidhi mfano wa hundiMzee Emmanual Shayo kutoka Pugu Dar es Salaam ambaye alijishindia milioni 27


Meneja Mawasiliano kampuni ya michezo ya kubahatisha ya TatuMzuka,Sebastian Maganga alisema kuwa wanayo furaha kubwa ya kuwatambulisha washindi wawili wa Tatumzuka waliopatikana tarehe 21 Januari 2018, jumapili iliyopita kupitia Mzuka Jackpot ambayo pia ilirushwa moja kwa moja kupitia vituo vya ITV, Clouds TV na TV1.

Maganga aliwataja washindi hao kuwa ni Mzee Emmanual Shayo kutoka Pugu Dar es Salaam ambaye alijishindia milioni 27,Mshindi mwingine alikuwa ni Britony Mtalemwa ambaye ametokea Songea,ambaye alijishindia milioni 40.

"Washiriki wa wiki hii walichukua jumla ya milioni 134 kwa pamoja. Washindi wengine wa wiki hii walikuwa ni Gibson Erasmas kutoka Mwanza aliyeondoka na milioni 40 na Andrew Kagoma kutoka Arusha aliyejinyakulia milioni 27'alisema Maganga..

Amesema Tatu Mzuka inawawezesha Watanzania wengi zaidi kutoka sekta mbalimbali na mikoa tofauti kuliko mchezo mwingine wowote. Kama Tatu Mzuka, amini kwamba tunatafuta njia zaidi kukupa fursa ya kuwa milionea kwa kiwango cha chini kabisa cha shilingi 500.Kila saa ndani ya siku, Tatu Mzuka inakupa fursa ya kushinda hadi milioni 6.Kila siku, siku sita za wiki kuanzia Jumatatu hadi Jumamosi tuna droo ya milioni 10 inayoitwa ‘Mzuka Deile’.

"Na Jumapili ya wiki hii, tuna milioni 60 ambayo inatafutiwa mshindi,Nafasi hizi zote zinapatikana kwako kwa kiasi cha shilingi 500 tu''alimaliza kusema Maganga.

“HALMASHAURI ISIYOPANDA MITI MILIONI 1.5 MWAKA HUU KUTOZWA FAINI,” RC WANGABO.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mwenyekiti wa Tasisi ya REYO Abdallah Rubega (Flana Nyeupe) akitoa maelezo juu ya aina ya miti itakayopandwa katika msitu wa Wangabo kwa heshima ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa mazingira huku ameshikilia bango la kuhamasisha wananchi kuacha kuchoma moto misitu na kuendelea kutunza vyanzo vya maji. 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akipanda mti ishara ya kufungua upandaji miti Mkoani Rukwa iuli kufikia lengo la mkoa la kupanda miti milioni 6, Maadhimisho yaliyofanyika katika Shule ya Sekondari Matai, Wilayani kalambo.
Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dk. Khalfan Haule (kulia) akisaidiana na baadhi ya wananfunzi wa Shule ya Sekondari Matai kupanda miti ikiwa ni juhudi za kuwaelimisha wananfunzi umuhimu wa kupanda miti. 
Mmoja wa Wananfunzi wa Shule ya Sekondari Matai, Joseph Katepa akiwa amepumua baada ya kupanda miti kadhaa katika eneo lililoandaliwa maalum kwa kupanda miti katika shule hiyo.
Wanafunzi mbalimbali wakiendelea kupanda miti  katika eneo lililoandaliwa maalum kwa kupanda miti katika shule hiyo. 
  ​
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ameziagiza Halmashauri nne za Mkoa wa Rukwa kuhakikisha zinafikia lengo la kupanda miti milioni 1.5 kila moja hadi kufikia mwisho wa mwaka wa 2017/2018 ili kufikia lengo la Mkoa la kupanda miti milioni 6 katika kutekeleza sera ya kupanda miti kitaifa.

Amesema kuwa Halmashauri itakayoshindwa kufikia lengo itatakiwa kulipa faini ya shilingi Milioni 1 kuilipa Halmashauri itakayofika lengo ambapo Halmashauri Mshindi inategemewa kupata shilingi Milioni 3 na fedha hizo itapewa taasisi itakayopanda miti mingi kuliko taasisi nyingine ya serikali ndani ya Halmashauri iliyoshinda hasa mashule ili kuwafundisha wanafunzi umuhimu wa kupanda miti.

“Halmashauri ambayo haikufikia lengo imuume kutoa shilingi Milioni 1 kumlipa mwenzake, katika hizo Halmashauri 4, kwa maana mshindi atapata shilingi Milioni 3, lakini endapo Halmashauri zote zitafikia malengo nitazipa Halmashauri Shilingi Milioni 1, na hiyo fedha itakwenda kwenye taasisi iliyopanda miti mingi kuliko taasisi nyingine hasa mashule,” Mh. Wangabo alibainisha.

Ameongeza kuwa mwaka ujao wa 2018/2019 halmashauri itakayoshindwa kufikia lengo la kupanda miti Milioni 1.5 italipa faini ya shilingi Milioni 5 ili kila halmashauri iweze kufikia lengo na kutimiza maelekezo ya serikali na kuwaonya wote wenye tabia ya kuchoma misitu jambo linalokwamisha jitihada za kutunza mazingira.

Ameyasema hayo alipokuwa akizindua wiki ya kupanda miti  Kimkoa iliyofanyika katika katika Shule ya Sekondari Matai, Wilaya ya kalambo ambapo miti 100 ilipandwa katika uwanja uliopewa jina la Msitu wa Wangabo kama kuunga mkono juhudi za Mh. Joachim Wangabo katika kuhakikisha kuwa Mkoa wa Rukwa haubaki kuwa jangwa hasa kwa kilimo kinachotegemea mvua.

Nae akisoma risala Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Mh. Julieth Binyura kabla ya kumkaribisha Mh. Wangabo alisema kuwa miongoni mwa mikakakti iliyowekwa na Wilaya hiyo ni kuhakikisha kila Kaya inapanda miti mitano na kuhakikisha kila shule inatenga eneo la kupanda miti ya matunda na mbao.

Pia alitumia nafasi hiyo kutoa takwimu za miti iliyopandwa na Wilaya hiyo, “kwa mwaka 2016/2017 miti 497,896 ilipandwa na kwa mwaka 2017/2018 mategemeo ya Wilaya ni kupanda miti Milioni 1.5 pamoja na changamoto za mifugo pamoja na wananchi kukosa hamasa ya kupanda miti tutahakikisha tunatoa elimu na kutenga bajeti kwaajili ya shughuli hiyo,” Alisema.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dk. Khalfan Haule amesema kuwa mkakati wa Wilaya ni kuhakikisha kila mwanafunzi kwa shule za msingi na sekondari anapatiwa mti na uongozi wa shule autunze na ukivunwa asilimia 40 atapewa mwanafunzi na asilimia 60 itabaki shuleni.

Nazo taasisi mbalimbali za utunzaji wa mazingira wameahidi kushirikiana na Halmashauri katika kutoa elimu na kuwa na vijiji vya mfano ambavyo wanakijiji wanaweza kutoa ushuhuda juu ya elimu ya mti waliyoipata na faida mabazo zimepatikana kutokana na wingi wa miti watakayokuwa nayo katika vijiji.

 Kwa mwaka 2016/2017 Mkoa wa Rukwa ulipanda miti 2,489,296 ambayo ni sawa na asilimia 41.5 ya lengo na mwaka 2017/2018 hadi sasa Mkoa umepanda miti 2,173,649 ambayo ni sawa na asilimia 36.22.

Wakulima na Wasambazaji mbolea Rukwa Waridhishwa na upatikanaji wa mbolea hadi vijijini.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mmoja wa Wajumbe wa Kamati ya ulinzi na Usalama ya Mkoa, Kamanda wa Zimamoto Mkoani Rukwa akikagua mbolea katika ghala la Kampuni ya Mbolea ya Taifa (TFC) lililopo Sumbawanga Mjini. ​
Mmoja wa Wasambazaji wakubwa wa mbolea Mkoa wa Rukwa Mohamed Mdanga (Kulia) akitoa maelezo ya upatikanaji wa mbolea Mkoani humo mbele ya Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo(kushoto) alipokwenda kumtembelea kwenye ghala lake na kukuta mbolea zai ya tani 300.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (wa mbele wa kwanza kushoto)alipokuwa akipita mtaa kwa mtaa katika mji wa Sumbawanga kujionea biashara ya mbolea inavyokwenda katika maduka ya mbolea (hayapo pichani) huku akiwa ameambatana na Meya wa manispaa ya Sumbawanga Mh. Justin Malisawa (koti la Draft).
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (wa pili kutoka kulia) akiwa amesimama mbele ya duka la mbolea kuulizia upatikanaji wa bidhaa hiyo katikati ya mji wa sumbawanga, Mkoani Rukwa.
Timu ya wataalamu wa Kilimo, Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na Viongozi wa Manispaa ya Sumbawanga, wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa kupita duka hadi duka kujionea upatikanaji wa mbolea katika mkoa wa Rukwa.



Wafanyabiashara wakubwa wa mbolea Mkoani Rukwa pamoja na wakulima wameridhishwa na upatikanaji wa mbolea na kusifu juhudi za serikali baada ya kupaza sauti zao na kusikika na Rais Dk. John Pombe Magufuli na jambo hilo kufanyiwa kazi ndani ya muda mfupi.

Wafanyabiashara hao wamesema kuwa wakulima hivi sasa hawapangi tena foleni kusubiri mbolea iliyokuwa ikipatikana kwa taabu na kwa kunyang’anyiana na kuwa foleni hizo zimekwisha na wakulima hawana haja ya kutoka Kijiji kuja mjini kufuata mbolea kwani mbolea hizo zinawafuata huko waliko hasa baada ya marekebisho ya bei elekezi iliyotolewa na Uongozi wa mkoa wa Rukwa chini ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo.

Mmoja wa Wafanyabiashara hao wakubwa Mohamed Rashid Mdangwa wa Kampuni ya ETG amesema “Sasa wakulima wameanza kupata mbolea kwa wingi, mwanzo walikuwa wanapanga foleni hapa lakini kuanzia ile Jumatatu agizo la Rais kuwa mbolea iende Mkoa wa Rukwa, sasa hivi population (wingi) ya watu imepungua sana, sasa hivi mahitaji ya mbolea sio makubwa sana kama miezi miwili iliyopita,na mbolea ipo nyingi njiani inakuja, na bei elekezi aliyoitoa Mkuu wa Mkoa imesaidia mbolea kufika vijijini kupitia wakala wadogo wa mbolea.”

Yamewsemwa hayo baada ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akiongozana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa kupitia maghala makubwa ya mbolea yaliyopo Sumbawanga Mjini pamoja na baadhi ya wasambazaji wadogo ili kujionea upatikanaji wa mbolea hizo tangu kutolewa kwa agizo la Rais Dk. John Pombe Magufuli la kusambaza mbolea hizo katika Mikoa inayoongoza kwa uzalishaji wa chakula nchini tarehe 8.1.2018.

Mh. Wangabo aliwasihi wasambazaji wadogo wa mbolea kuendelea kujitokeza na kununua mbolea hiyo ambayo bei iliyopo sasa imezingatia maoni yao na haiumizi, hivyo kufanya hima kuhakikisha kuwa mkulima hakosi mbolea ili kuweza kubaki katika lengo la kuzalisha chakula kwa wingi na kuleta ushindani na mikoa mingine inayozalisha chakula.

“Mimi nitoe wito tu kwa wale Agrodealers (wasambazaji wadogo wa mbolea) wafike kuendelea kununua mbolea, hata bei tumekwishazifikiria tena upya, kila Halmashauri katika Wilaya wamekwisha kaa na kutoa mapendekezo yao halisi ya kiusafirishaji, kwahiyo wafike wanunue mbolea na kutakuwa na faida, bei imezingatia hadi miundombinu iliyoharibika hakutakuwa na usumbufu,” Mh. Wangabo alifafanua.

Mh. Wangabo alitembelea maghala matatu ya wafanyabiashara wakubwa waliopo mjini sumbawanga, TFC pamoja na maduka ya wasambazaji wadogo matatu na kuongea na baadhi ya wakulima ili kujithibitishia upatikanaji wa mbolea hiyo kwa maeneo ya mjini na inayopelekwa vijijini.

Kwa msimu wa 2016/2017 Mkoa wa Rukwa ulilima Hekta zipatazo 556,975.9 na kuvuna tani 1,109,055.6 za mazao ya chakula kati ya hizo mahindi yalikuwa tani 710,602. Kwa msimu huu wa Kilimo wa 2017/18 Mkoa umelenga kulima jumla ya eneo la Hekta 554,310.6 na kuvuna tani 1,669,746.2 za mazao ya chakula.

SERIKALI YAANZA KUTUMIA MFUMO WA NYOTA KATIKA KUVIPIMA VITUO VYA AFYA NA HOSPITALI NCHINI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Naibu Waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (MB) akikagua Bin Kadi ambayo inaonesha idadi ya Dawa zilizoingia na zilizobaki katika stoo ya dawa ya Kituo cha Afya Nkomolo Mkoani Rukwa.
 Naibu Waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (MB) akikagua jokofu la Chanjo wakati alipotembelea katika Kituo cha Afya cha Nkomolo kilichopo Nkasi Mkoani Rukwa wakati wa Ziara yake ya kukagua Huduma za Afya Mkoani Rukwa.
 Naibu Waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (MB) akikagua Idadi ya watu waliohudhuria Kituoni hapo kupitia mfumo wa Kompyuta katika stoo ya dawa ya Kituo cha Afya Nkomolo Mkoani Rukwa.

Naibu Waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (MB) akipokea maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa Majengo Mhandisi Mwakyembe kutoka Ofisi ya Mkoa wa Rukwa.

 Naibu Waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (mwenye tisheti ya mistari) akipokea maelekezo ya ramani ya jingo jipya la Mama na Mtoto katika kituo cha Afya Nkomolo, anaemfuatia ni Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Boniface Kasululu na wa mwisho ni Mhandisi Mwakyembe.
Naibu Waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiendelea na ziara yake katika kituo cha Afya Nkomolo, anaemfuata ni Mhandisi Mwakyembe na Mbunge wa Nkasi kaskazini Mh.Kessy Ally.



Na WAMJWW. RUKWA-NKASI

Serikali yaanza kutumia mfumo wa nyota kupima huduma zitolewazo na Vituo vya Afya, Hospitali na Zahanati nchini ili kupima utendaji kazi wa watumishi wa Sekta ya Afya katika kutoa huduma kwa wananchi.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipotembelea Kituo cha Afya cha Nkomolo Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa, ikiwa ni muendelezo wa Ziara yake ya kukagua shughuli za utoaji wa huduma za Afya na kuamsha hali kwa wananchi katika kujihusisha na shughuli za maendeleo katika maeneo yao.

“Tumeanza utaratibu wa kutoa nyota katika vituo vya Afya, imeanzia nyota sifuri mpaka nyota tano, sifuri maana yake kituo hicho hakifai kutoa huduma ya Afya na nyota tano maana yake kinafanya vizuri sana” Alisema Dkt. Ndugulile.

Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile aliridhishwa na hali ya upatikanaji wa Dawa katika kituo hicho, hivyo kuwatoa hofu wananchi na kusisitiza kuwa hawapaswi kuuziwa dawa zote muhimu kwani Serikali imeboresha hali ya upatikanaji wa Dawa katika vituo vyote vya Afya nchini.

“Dawa zote za msingi tunazo zakutosha, hivyo hatutarajii kuona mtu aje hapa kutibiwa kisha aambiwe akanunue katika vituo binafsi, Hali ya upatikanaji wa Dawa ni nzuri katika kituo hiki na ni asilimia 85 ” aliendelea Dkt. Ndugulile.

Aidha, Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kaskazini Mh. Ally Kessy aliupongeza uongozi wa Mkoa kwa kusimia vizuri ujenzi wa kituo hicho, uliojumuisha Thieta, Wodi ya mama na mtoto mochwari na maabara mpaka hatua ya kupaua kwa jumla ya kiasi cha shilingi Bilioni 290 kwa kutumia nguvu kubwa ya wananchi (fixed akaunti).

Akiwasilisha taarifa ya Mkoa, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt Boniface Kasululu amesema kuwa Mkoa wa Rukwa umeendelea kuboresha huduma za Afya ya mama na mtoto katika maeneo ya vijijini kama juhudi za kupunguza tatizo la vifo vya wanawake na watoto wachanga vitokanavyo na matatizo ya uzazi.

Dkt. Boniface aliendelea kusema kwamba, Zaidi ya vituo 214 kati ya 223 vilivyopo, vinatoa huduma muhimu za mzazi na mtoto jambo linalosaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na watoto wachanga licha ya upungufu mkubwa wa vituo hivyo.

Kwa upande mwingine Dkt. Boniface Kasululu alisema kwamba Mkoa unaendelea kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kuwapeleka watoto katika vituo vinavyotoa huduma za chanjo, Hadi kufikia Mwezi Novembe 2017 jumla ya Watoto 48,494 wenye umri wa chini ya mwaka mmoja walipewa chanjo, kati ya watoto 50,245 waliotarajiwa ambao ni sawa na asilimia 96 jambo lililoufanya mkoa kuvuka lengo la kitaifa la asilimia 90.

MVUA KUBWA YASABABISHA WATU KUKIMBIA JENEZA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
 
Na   Walter  Mguluchuma
Nkasi
HALI ya Taharuki na hofu imezuka katika kijiji cha Katani kata ya Nkandasi wilayani Nkasi mkoani Rukwa na kupelekea waombolezaji kutimua mbio na kuacha jeneza lenye mwili wa marehemu baada ya mvua kubwa kuanzakunyesha na kubomoa nyumba za wakazi wa kijiji hicho.

Tukio hilo lilitokea Juzi majira ya saa 6 mchana mara baada ya kuanza kunyesha mvua kubwa zilizoambatana na radi na upepo mkali ulioezua baadhi ya nyumba za wanachi hao ambao walikuwa wakiomboleza msiba wa mwananchi mwenzao aliyefaniki baada ya kuugua siku chache zilizopita. 

Akizungumza na gazeti hili mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Kaungo, Robert Kanoni alisema kuwa wakiwa wanaelekea kufanya maziko ya marehemu Dismas Kanoni aliyefari Jana, ghafla ilianza kunyesha mvua kubwa ikiambatana na radi na upepo mkali hali iliyosababisha baadhi ya waombolezaji kutimua mbio na kurejea majumbani kutokana na hofu iliyoibuka kufuatia tukio hilo.

Baadhi ya wananchi walivumilia nakurejea na jeneza lililokuwa na mwili wa marehemu nyumbani na kuahilisha maziko kwamuda ili kupisha hali hiyo uweze kutulia na walikwenda kuzika baadaye katika makaburi yaliyopo kijijini hapo. 

Alisema kuwa tukio hilo limezua hisia za kishirikina  kwa wananchi wa kijiji hicho kwani miezi miwili iliyopita baba yake na marehemu huyo alifariki baada ya kugongwa na gari la kampuni ya ujenzi wa barabara na walipofanya maziko siku iliyofuata walikuta ngozi ya kondoo juu ya kaburi la marehemu kitendo kilicho washangaza wakazi hao.

Kanoni alisema kuwa kutokana na mvua hiyo nyumba zipatazo 10 zimebomoka kabisa na zinatakiwa kujengwa upya huku nyumba nyingine Saba,  zikiwa zimeezuliwa paa na kuwaacha wakazi wake wakiwa hawana sehemu ya kukaa licha ya kuwa wamepata hifadhi na misaada ya kibinaadamu kwa wenzao.  

Naye Peter Kalale mkazi wa kijiji hicho akizungumzia tukio hilo  alisema kuwa mara kwa mara kijiji hicho kimekuwa kikikumbwa na dhoruba pindi mvua zinaponyesha kwakua kimepitiwa na mkondo wa upepo mkali ambao unasababisha hali hiyo. 

Alisema changamoto iliyopo ni tabia ya wananchi kukata miti kwaajili ya mashamba  na hivyo kusababisha pepo zinapovuma hazikuti kizuizi chochote na hivyo imekuwa sababu ya kuezuliwa nyumba zao na hata kubomoka kabisa. 

Kwaupande wake mwenyekiti wa kamati ya maafa ya wilaya hiyo ambaye ni mkuu wa wilaya  hiyo Said Mtanda ilikiri kutokea kwa tukio hilo na kutoa wito kwa wananchi kujenga makazi bora kwani miongoni mwa nyumba  hizo zipo ambazo zimeezekwa kwa nyasi.

Alisema kuwa sera ya serikali ya awamu ya tano ni  kuwahimiza wananchi wajenge nyumba bora na zakisasa ili waweze kuepuka majanga yanayotokana na tabia nchi kwani bila kufanya hivyo wananchi wataendelea kupata hasara.


KATEKISTA AFARIKI BAADA YA KUENDESHA IBADA YA MAZISHI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Imeandikwa na Peti Siyame, Tanganyika
MWALIMU wa dini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mpanda, Noel Sitemele amefariki dunia muda mfupi baada ya kumaliza kuongoza ibada ya mazishi ya muumini wake yaliyofanyika katika makaburi ya Mchakamchaka Kijiji cha Majalila wilayani Tanganyika mkoani Katavi.
Katekista huyo alikuwa akitoa huduma ya kiroho katika Kigango cha Mchakamchaka kilichopo katika Parokia ya Mpanda Ndogo katika Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi. Akizungumzia mkasa huyo, Diwani wa Kata ya Mpanda Ndogo, Hamad Mapengo alisema licha ya Sitemele kuwa mwalimu wa dini, katika uhai wake alikuwa pia Mwenyekiti wa Kijiji cha Majalila kilichopo katika Halmashauri ya Mpanda wilayani Tanganyika.
Mapengo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mpanda, alisema Katekista alifariki dunia juzi saa 11 jioni muda mfupi baada ya kufikishwa zahati ya kijijini Majalila kutibiwa.Alisema kabla ya kukutwa na umauti, Katekista huyo alikuwa mwenye siha njema na aliongoza ibada ya mazishi ya muumini wake hadi mwisho katika makaburi ya Kigango cha Mchakamchaka kilichopo katika Kijiji cha Majalila ambapo alianza kujisikia vibaya.
“Baada ya kumaliza ibada hiyo ya mazishi, alianza kujisikia vibaya hivyo akalazimika kurejea nyumbani kwake na kuwaacha waombolezaji makaburini,” alieleza Mpaengo. Alisema, baada kufika nyumbani kwake, hali yake iliendelea kuwa mbaya na aliomba msaada kutoka kwa majirani zake wamkimbize kwenye kituo cha afya kwa matibabu.
Inaelezwa zahanati hiyo haiko mbali kutoka alikokuwa akiishi mwalimu huyo wa dini. Mwenyekiti alisema, taarifa za kifo cha Katekista huyo zilizagaa haraka kijijini humo na kuwafikia waombolezaji waliokuwa nyumbani kwa marehemu aliyeongozewa ibada ya mazishi na Katekista huyo waliopata simanzi kubwa wengine wakiwa hawaamini jambo hilo.
Maziko yake yalifanyika jana makaburi ya kigango cha Mchakamchaka Kijiji cha Majalila. Padri Paschal Kipenye wa Parokia ya Mpanda Ndogo aliongoza ibada ya mazishi yaliyohudhuriwa na mamia ya waombolezaji akiwemo Mbunge wa Mpanda Vijijini, Selemani Kakoso.
CHANZO HABARI LEO 

RC WANGABO AZIHIMIZA HALMASHAURI KUONGEZA MASHINE ZA MAPATO KUONGEZA UKUSANYAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dk. Khalfan Haule akitoa maelezo ya kumtambulisha Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo kwa wananchi wa kijiji cha Zimba kata ya Mtowisa, Wilayani Sumbawanga. wakati walipofika kwenye kijiji hicho kuona kiwanda cha kukamulia alizeti. 
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (wa tatu kutoka kulia) akiuliza swali kwa mhandisi wa maji wa Wilaya Patrick Ndimbo (wa kwanza kushoto) wakati walipotembelea mradi wa maji wa kutumia umeme wa jua mji mdogo Laela Wilayani Sumbawanga wenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.8. 
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akishiriki kutumia ala ya kigoda kuchekecha juu ya mtungi na kuzalisha sauti inayowezesha kuleta mlio kwaajili ya kunogesha nyimbo, Ni ala ya asili inayotumiaka katika ngoma za kitamaduni za Kifipa muda mfupi kabla ya kufanya mkutano na wananchi wa mji mdogo wa Laela. 
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akimsalimia mmoja wa kinamama wa kikundi cha ngoma Laela Odila Maufi wakati alipokuwa akiingia katika viwanja vya shule ya Msingi Laela kwaajili ya Mkutano wa hadhara kujitambulisha kwa wananchi na kuongea nao.  


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewasifu wananchi wa kata ya Mtowisa, Tarafa ya Mtowisa, Wilayani Sumbawanga kwa kuonyesha mshikamano katika ujenzi wa shule ya Sekondari Vuma pamoja na ujenzi unaonendelea wa kituo cha polisi kitakachohudumia tarafa ya mtowisa.

Tarafa hiyo yenye kata 4 ina shule moja ya kidato cha tano na sita jambo alilosifu Mh. Wangabo kuwa imetimiza ilani cha Chama Tawala kwa kuwa na Shule moja ya aina hiyo kwa kila tarafa.

Amesema kuwa ataendelea kusisitiza kauli ya serikali ya awamu ya tano ya kuwa maendeleo hayana vyama, hivyo alisisitiza wananchi hao kutobaguana kwa itikadi zao bali wahimizane katika kutatua changamoto na kuleta maendeleo katika tarafa yao.

“Mmenivuti mliponieleza kwamba mnashirikiana katika nyanja mbalimbali, kuna majengo yale ya shule mnashirikiana na jengo hili la polisi mnashirikiana ili kuhakikisha kwamba changamoto mbalimbali zilizopo ndani yenu mnazitatua, hili limenifurahisha na ningependa muendelee nalo, na umeoja na mshikamano uliopo muudumishe bila ya kujali vyama vyenu.” Alisifu.

Ameyasema hayo katika Mkutano wa hadhara katika Kijiji cha mtowisa, kata ya mtowisa Wilayani Sumbawanga katika ziara yake ya siku mbili katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga yenye lengo la kutembelea miradi mbalimbali na kujitambulisha kwa wananchi.

Kwa upande wake diwani wa Kata ya mtowisa Mh. Edgar Malini alisema kuwa wananchi wa mtowisa hawana tabu wa kutoa ushirikiano ili kujiletea maendeleo wenyewe isipokuwa wamekuwa na kilio cha muda mrefu kuhusu umeme na maji.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa