Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa, Mh. Joachim Wangabo akifafanua namna mtumishi
anavyotakiwa kuwajibika pindi anapowahudumia wananchi (aliyekaa) kaimu
Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa David Kilonzo.
Viongozi
wa mashirika ya ya umma na mamlaka mbalimbali za seikali Mkoani Rukwa
Waliohudhuria kwenye kikao hicho kilichowakutanisha wakuu wa mamlaka na
mashirika ya umma.
Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa, Mh. Joachim Wangabo amewaasa watumishi wa mashirika
ya umma na wakala wa serikali mkoani Rukwa kutotumia vyeo vyao
kuwanyanyasa wananchi wanaowahudumia na badala yake wawasaidie kwa
kuzingatia misingi ya haki na usawa bila ya kujali, rangi kabila, dini
na hali zao kiuchumi.
Amesema
kuwa watumishi wa serikali ni watumishi wa wananchi hivyo wanapaswa
kujituma bila ya kujali vyeo vyao kwani vyeo hivyo havitakuwa na maana
ikiwa wananchi hawapati huduma wanayoitarajia kutoka katika serikali
waliyoiweka madarakani.
“Sisi
viongozi wa Serikali lazima tufanye kazi kwa kujituma na kujitoa na
tukumbuke kuwa sisi ni watumishi tu, sio watu wa kujivuna ama wabinafsi
na kujinadi kwa vyeo vyetu kwamba mimi meneja, daktari sijui nani, vyeo
vyetu vitakuwa na maana pale tu tunapokwenda kwa wananchi na kuwapa
huduma” Alieleza.
Na
kuongeza kuwa serikali ya awamu ya tano ipo kuhakikisha kuwa kila
kiongozi anayehudumia wananchi anakuwa mtumishi wa wananchi na
kuhakikisha kuwa haki inatendeka na kuonya vikali watumishi
wanaowahudumia wananchi kwa kutumia lugha chafu.
Ameyasema
hayo kwenye kikao cha muda mfupi kilichowajumuisha viongozi kutoka
katika mashirika ya umma, wakala na mamlaka mbalimbali za serikali
zilizomo Mkoani humo ili kufahamu matatizo wanayokumbana nayo pindi
wanapotimiza wajibu wao wa kuwahudumia wananchi.
Sambamba
na hayo Mh. Wangabo amewataka watumishi wote Mkoani humo kuzingatia
muda na kutekeleza kwa wakati mipango waliyojiwekea ili kazi zizae
matunda na kutoa taarifa sehemu husika bila ya kusubiri kusukumwa.
0 comments:
Post a Comment