Home » » MWANAMKE ACHARANGWA MAPANGA, ACHINJWA

MWANAMKE ACHARANGWA MAPANGA, ACHINJWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Imeandikwa na Peti Siyame, Nkasi
MWANAMKE mkazi wa Kijiji cha China Kata ya Kate, Nkasi, Rukwa, Telestina Silanda (45) ameuawa kwa kuchinjwa na mwili kucharangwa na watu wasiojulikana akiwa amelala nyumbani kwake usiku wa kuamkia jana.
Ndugu wa marehemu, Charles Silanda alidai tukio hilo lilitokea saa mbili usiku watu wasiojulikana waliovalia “kininja” walipovamia nyumba yake (shangazi) na kumshambulia kwa panga na kumchinja.
Alisema hadi wao wanajulishwa tukio hilo na kukimbilia eneo la tukio walikuta shangazi ameuawa na wauaji hao wametoweka katika eneo la tukio. Ofisa Mtendaji wa kijiji hicho, Konrad Kauzeni alisema mwanamke huyo aliuawa kinyama, kwa kukatwa miguu yake yote miwili na kuitenganisha na mwili, kichwa na shingo.
Alisema mume wa mwanamke huyo alikuwa amekwenda porini kurina asali kwenye mizinga yake na aliporejea nyumbani alikuta mkewe kauawa kikatili na waliofanya tukio hilo hawajafahamika.
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Said Mtanda ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo akisema ataenda kijiji hicho wananchi wapige kura za maoni ili kuwabaini wauaji hao.
Alisema ni jambo lisilokubalika watu kufanya uhalifu mkubwa kiasi hicho na wakaachwa, hivyo kura za maoni zitasaidia kuwanasa wauaji hao ili sheria ichukue mkondo wake. Aliwataka wakazi wa eneo hilo kwenda ofisini kwake kutoa taarifa za siri kwa wale wanaowafahamu.
CHANZO HABARI LEO
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa