Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akitoa nasaha kwa wazee wa Mkoa wa
Rukwa na waandishi wa habari (hawapo pichani) alipokwa akizungumza na
wazee hao.
Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewatahadharisha wakuu wa Wilaya
na wapenda maendeleo wote Mkoani Rukwa wasiwanyanyase waandishi wa
habari pindi wanapohitaji habari za kutangaza fursa zilizomo katika
Mkoa.
Ameonya
kuwa kuna baadhi ya viongozi wamekuwa wazito kutoa ushirikiano kwa
waandishi wa habari jambo linalopelekea wadau wa maendeleo walio nje ya
Mkoa kutofahamu fursa zilizomo katika mkoa na changamoto zinazopatikana
ili watoe ushirikiano katika kuzitatua changamoto hizo.
“Kwa
Mkoa huu wa Rukwa waandishi wa habari Ruksa kufanya kazi yenu vizuri,
Vyombo vya habari ni fursa, wao ndio watakaoiambia dunia kuwa Rukwa iko
hivi, hakuna mwandishi atakayewekwa ndani katika mkoa huu, wao ni wadau
muhimu sana katika maendeleo na sio watu wa kuwaweka pembeni katika
kufikisha ujumbe kwa jamii,” alisisitiza
Ameyatamka
hayo wakati wa kikao chake na wazee wa Mkoa wa Rukwa pamoja na baadhi
ya viongozi wa dini kilichowaalika waandishi wa habari ili kuijua
mipango na mikakati yake katika kuonafursa za Rukwa zinatangazwa
kitaifa na kimataifa.
Lakini
pia hakusita kuwatahadharisha waandishi hao kuwa anayekwenda kinyume na
miiko ya uandishi na kugeuza misingi ya kazi yake, hatokuwa na nafasi
ya kufanya kazi katika Mkoa na kuongeza kuwa mwandishi wa habari hapaswi
kuwa wakala wa vyama vya kisisasa na kuacha kuandika mazuri
yanayotendwa na serikali ya awamu ya tano.
0 comments:
Post a Comment