NG’OMBE
wapatao 692 ambao ni miongoni 1,332 walioshikiliwa na kuzuiliwa
katika Hifadhi ya Pori la Akiba la Rukwa – Lukwati kwa zaidi ya mwaka
mmoja wamekufa kwa kukosa matunzo bora imefahamika
.
Kufuatia
hilo Waziri wa Mifugo na Uvuvi ,Luhaga Mpina ameagiza uongozi wa
hifadhi hiyo kurejesha mara moja ng’ombe waliosalia wapatao 640 ambao
ni mali ya wafujaji watatu kwa kuwa wanashiliwa kinyume cha sharia .
Waziri
Mpina alitoa agizo hilo wakati alipotembelea hifadhi hiyo iliyopo
katika Bonde la Ziwa Rukwa wilayani Mlele mkoa wa Katavi kwa lengo la
kutatua mgogoro wa muda mrefu baina ya wafugaji hao watatu na uongozi wa
hifadhi hiyo .
Alisema
kuwa ameshutushwa na taarifa iliyosomwa na Meneja wa Hifadhi hiyo ,
Paschal Mhina ambapo alimweleza kuwa ng’ombe wapatao 1,332 waliovamia
hifadhi walikamatwa na kushikiliwa kwa mwaka mmoja na miezi tisa
ambapo ng’ombe wapatao 692 wameshakufa na waliobakia ni 640 .
Aidha
aliuagiza uongozi wa Serikali ya mkoa wa Katavi kuhakikisha
inahakikia mifugo hiyo na kuwakabidhi wenye mali kwamba wale wote
watakaobainika kusababisha vifo vya ng’ombe hao waliokufa kwa uzembe
wachukuliwe hatua kali za kinidhamu na kijinai .
“
Hakukuwa na sababu yoyote ile ya msingi ya
kuendelea kuishilikia mifugo hiyo baada ya wenye mali hiyo kufungua
mashitaka mahakamani ambapo katika kesi ya awali watuhumiwa watau
ambao ndio mwenye mai hiyo walifungua mashataka katika
katika Mahakama ya Wilaya ya Mpanda ambapo mahakama hiyo
iliamuru itaisishwe na iwe mali ya Serikali” alieleza .
Alimtaka Meneja
wa pori la Akiba amwonyeshe hati yoyote inayowapa mamlaka
ya kuendelea kuwashikili ngombe hao wakati wafugaji walikuwa w anatuhumiwa walikata rufaa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga kupiga kutaifishiwa ngombe zao .
Alisema
isitoshe Mahakama Kuu ilitengua hukumu iliyotolewa na Mahama
ya Wilaya ya Mpanda na kuamuru wafugaji hao watatu warejeshewe mifugo
yao na faini ya Sh 500,000/- walizotozwa .
Wafugaji hao watatu ni pamoja na Shigela Mayunga , Charles Mtokambali na Kelenja Makuja .
“Nimesikishwa sana
na kitendo cha uongozi wa hifadhi ya pori la akiba la Rukwa – Lukwati
kwa kuendelea kuishikilia mifugo hiyo ambapo idadi kubwa ya mifugo
hiyo imekufa kwa magonjwa ….nataka kujua kwanini mifugo waliendelea
kushikiliwa ndani ya hifadhi hiyo likiwa ni eneo maalumu lililotengwa
kwa ajili ya wanyamapori na sio ng’ombe “ alihoji kwa hisia .
Kwa upande wake Meneja wa Pori la Akiba la Rukwa Rukwat i Mhina alieleza kuwa mifugo hiyo ilendelea kushikiliwa kwa kile alichodai kuwa baada ya uongozi wa hifadhi hiyo kukata rufaa kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga Sumbawanga.
Aliongeza
kuwa ungozi wa hifadhi hiyo ulipewa maelekezo na Mwanasheria wa
Serikali kuwa waendelea kuitunza mifugo hiyo kama sehemu ya kielelezo
cha kesi hiyo ..
Kwa
upande wake , Katibu Mkuu wa Chama cha Wafugaji Tanzania Makoye
Nkonosinema alisema kuwa mifugo iliyokufa ikiwa mikononi mwa uongozi
wa hifadhi hiyo wataendelea kuidai .
Aidha
alitaka kupewa maelezo ya kina katika kipindi hicho chote ambacho
ng’ombe hao walikuwa wameshikiliwa ni ndama wangapi waliozaliwa .
Nae Ofisa
Utafiti wa Magonjwa ya Mifugo wa Mikoa wa Katavi na Rukwa , Protus
Reshola alisema kuwa idadi hiyo ya ng’ombe iliyokufa ni kubwa sana
kwamba imesababishwa na dosari kadhaa ikiwemo waliokuwa wakiwachunga
walikuwa sio wafugaji .
Aliongeza
kuwa kutopatiwa matibabu stahiki na kutokuwepo na josho kwenye hifadhi
hiyo kumesababisha ng’ombe hao kufa kutokana na ugonjwa wa homa ya
mapafu .
Habari imeandikwa na Walter Nguruchuma wa Rukwa yetu Blog
0 comments:
Post a Comment