Home » » NG'OMBE WAPATAO 692 WAMEKUFA BAADA YA KUKOSA MATUNZO BORA.

NG'OMBE WAPATAO 692 WAMEKUFA BAADA YA KUKOSA MATUNZO BORA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
NG’OMBE  wapatao  692 ambao  ni miongoni  1,332 walioshikiliwa na kuzuiliwa  katika Hifadhi ya Pori la Akiba la Rukwa – Lukwati  kwa zaidi  ya mwaka mmoja wamekufa kwa kukosa matunzo bora imefahamika
 .
Kufuatia hilo Waziri  wa Mifugo na Uvuvi ,Luhaga Mpina  ameagiza uongozi wa hifadhi hiyo kurejesha  mara moja  ng’ombe waliosalia wapatao 640 ambao ni mali ya wafujaji watatu kwa kuwa wanashiliwa kinyume cha sharia .
 
Waziri Mpina alitoa agizo hilo  wakati alipotembelea hifadhi hiyo iliyopo katika Bonde la Ziwa Rukwa wilayani Mlele  mkoa wa Katavi  kwa lengo la kutatua mgogoro wa muda mrefu baina ya wafugaji hao watatu na uongozi wa hifadhi hiyo .
 
Alisema kuwa ameshutushwa na taarifa iliyosomwa na Meneja wa Hifadhi hiyo , Paschal Mhina  ambapo alimweleza kuwa ng’ombe wapatao 1,332 waliovamia hifadhi walikamatwa  na kushikiliwa  kwa  mwaka mmoja na miezi tisa ambapo ng’ombe wapatao 692 wameshakufa  na waliobakia ni 640 .

 Aidha aliuagiza uongozi  wa Serikali ya mkoa wa Katavi kuhakikisha  inahakikia mifugo hiyo na kuwakabidhi wenye mali kwamba wale wote watakaobainika kusababisha  vifo vya ng’ombe hao waliokufa kwa uzembe wachukuliwe hatua kali za kinidhamu na kijinai . 
“ Hakukuwa na sababu yoyote  ile ya  msingi ya kuendelea  kuishilikia  mifugo hiyo baada ya  wenye mali hiyo kufungua   mashitaka  mahakamani  ambapo  katika kesi ya awali watuhumiwa watau ambao ndio mwenye mai hiyo  walifungua mashataka  katika  katika    Mahakama ya  Wilaya ya  Mpanda   ambapo  mahakama hiyo iliamuru  itaisishwe na  iwe  mali ya  Serikali” alieleza  .
Alimtaka   Meneja wa  pori la  Akiba  amwonyeshe  hati yoyote  inayowapa   mamlaka ya  kuendelea kuwashikili ngombe hao wakati  wafugaji   walikuwa  wanatuhumiwa  walikata rufaa   Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga  kupiga  kutaifishiwa  ngombe zao .
Alisema isitoshe  Mahakama Kuu  ilitengua  hukumu iliyotolewa na  Mahama ya  Wilaya ya Mpanda na kuamuru  wafugaji hao watatu warejeshewe  mifugo yao  na faini ya Sh  500,000/- walizotozwa  .
Wafugaji hao watatu  ni pamoja na Shigela Mayunga , Charles Mtokambali na Kelenja Makuja .
 “Nimesikishwa  sana na  kitendo cha  uongozi wa hifadhi ya pori la akiba la Rukwa – Lukwati kwa kuendelea kuishikilia mifugo hiyo  ambapo idadi kubwa ya  mifugo hiyo imekufa kwa magonjwa  ….nataka  kujua  kwanini mifugo  waliendelea kushikiliwa  ndani ya hifadhi hiyo  likiwa ni eneo maalumu lililotengwa  kwa ajili ya wanyamapori  na sio ng’ombe “ alihoji   kwa hisia .
Kwa upande wake  Meneja wa  Pori la   Akiba  la  Rukwa   Rukwati   Mhina  alieleza  kuwa mifugo hiyo ilendelea  kushikiliwa  kwa  kile   alichodai  kuwa   baada  ya uongozi wa hifadhi hiyo kukata rufaa kupinga hukumu iliyotolewa  na   Mahakama  Kuu  Kanda ya Sumbawanga   Sumbawanga.
Aliongeza kuwa ungozi wa hifadhi hiyo ulipewa maelekezo  na Mwanasheria wa Serikali  kuwa waendelea kuitunza mifugo hiyo  kama sehemu ya kielelezo cha kesi hiyo ..
Kwa upande wake ,  Katibu  Mkuu  wa  Chama cha Wafugaji  Tanzania Makoye Nkonosinema alisema kuwa mifugo  iliyokufa  ikiwa mikononi mwa uongozi wa hifadhi hiyo  wataendelea  kuidai .
Aidha alitaka kupewa maelezo ya kina  katika kipindi hicho chote ambacho ng’ombe hao walikuwa wameshikiliwa  ni ndama  wangapi waliozaliwa .
Nae  Ofisa Utafiti wa  Magonjwa ya   Mifugo wa  Mikoa wa Katavi  na Rukwa , Protus Reshola alisema kuwa idadi hiyo ya ng’ombe iliyokufa ni kubwa sana kwamba  imesababishwa na dosari kadhaa  ikiwemo waliokuwa wakiwachunga walikuwa sio wafugaji .
Aliongeza kuwa kutopatiwa matibabu stahiki na kutokuwepo na josho kwenye hifadhi hiyo  kumesababisha ng’ombe hao  kufa kutokana na ugonjwa wa homa ya mapafu .
Habari imeandikwa na Walter Nguruchuma wa Rukwa yetu Blog
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa