Home » » RC RUKWA APIGA MARUFUKU MAHINDI KUTOKA ZAMBIA

RC RUKWA APIGA MARUFUKU MAHINDI KUTOKA ZAMBIA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au W
Imeandikwa na Pety Siyame, Sumbawanga
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Joachim Wangabo.
MKUU wa Mkoa wa Rukwa, Joachim Wangabo amewapiga marufuku wafanyabiashara wanaoingiza mahindi kwa magendo kutoka Zambia na kuyauza kwa bei ya kutupa akitaka waache mara moja.
Wangabo alisema mahindi hayo yanayoingizwa kwa magendo mkoani Rukwa kutoka Zambia ndiyo yamesababisha kurundikana kwa mahindi lakini pia kuendelea kuanguka kwa bei ya mahindi yaliyovunwa na wakulima mkoani humo katika msimu huu wa kilimo na hivyo kuathiri soko lao.
Alipiga marufuku hiyo akijibu kilio cha wazee mkoani humo waliomweleza mahindi yamerundikana katika kila nyumba ya wakulima na wameshindwa kununua pembejeo za kilimo katika msimu huu.
“Kila nyumba imefurika mahindi, hakuna pa kuyapeleka kwa sababu ya kutokuwepo kwa soko la uhakika na la ushindani .... Basi tumebakia kula asubuhi, mchana na jioni hata zaidi ya mara nne ....wasiwasi tutashindwa kununua pembejeo za kilimo kwani fedha hatuna kila mtu analia tu ...pia kuna hatari wakulima wakashindwa kulima msimu huu,” Mzee Joseph Ngua alimweleza RC huyo.CHANZO HABARI LEO
hatsapp namba +255765056399.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa