Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
NAIBU Waziri wa Elimu Mhandisi Stella Manyanya amemuagiza
msimamizi wa ukarabati wa shule ya Sekondari Kantalamba kuhakikisha kuwa
walemavu wanajengewa vyoo vyao ndani ya mabweni wanamolalia nia ikiwa ni
kujiepusha na kuwaamsha wenzao usiku pindi wanapotaka kwenda chooni.Ametoa
agizo hilo leo jumapili (30/7/2017) muda mfupi baada ya kufanya ukaguzi wa
ukarabati wa shule hiyo iliyopo Wilayani Sumbawanga iliyopewa Shilingi Bilioni
1.1 ikiwa ni mpango wa serikali wa kuzirudishia hadhi shule kongwe nchini huku shule
hiyo ikiwa ni ya tangu 1964.
“Lazima muhakikishe kwamba Mnakuwa na vyumba maalum kwaajili ya
wanafunzi wenye ulemavu na kuwawekea miundombinu hasa kwa wale walemavu ambao
mazingira yao ni magumu Zaidi, kwa mfano mwanafunzi ana ulemavu wa miguu na anatakiwa
kwenda chooni hapaswi kutambaa kwenye mikojo ya wanafunzi wenziwe hii
inawapelea wao kuwa katika mazingira hatarishi zaidi,” Alisema.
Mbali na agizo hilo pia Mhandisi Manyanya ametoa wiki tatu
ukarabati wa shule hiyo kumalizika baaada ya muda waliopangiwa kumalizika huku
kipaumebele kikiwa ni kuhakikisha wanafunzi wanaendelea na masomo yao katika
hali ya utulivu.
“Sijaridhishwa na kasi ya ukarabati huu hivyo tumewaongezea wiki
tatu mhakikishe mnamaliza ili wanafunzi waendelee na masomo maana yake kama
mngekuwa hamwezi kumaliza kwa wakati kwanini msingesema mapema,” Alisisitiza.
Aidha alipokuwa anakagua bwalo la kulia wanafunzi aliagiza
kutanuliwa kwa bwalo hilo baada ya kuona kuwa bwalo hilo ni dogo na wanafunzi
ni wengi kiasi ambacho ingewabidi wanafunzi hao kula kwa zamu ili wote waweze
kulitumia bwalo hilo na kuongeza kuwa ukarabati unaofanyika ni pamoja na
utanuzi wa majengo kwani ukubwa wa jengo lililopo ni wa tangu 1964 na sasa ni
2017.
Kabla ya kumaliza ziara yake shuleni hapo aliwasisitizia
wanafunzi kuwa nia ya Serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha kuwa hakuna
tofauti kati ya shule za serikali na shule binafsi kuanzia huduma za majengo,
elimu na vifaa vya kusomea.
0 comments:
Post a Comment