Home » » Wauza kinyemela magogo ya milioni 50/-

Wauza kinyemela magogo ya milioni 50/-

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Hayo yamebainika wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Sumbawanga mjini, Aeshi Hilaly (CCM) aliyoifanya katika Hifadhi ya Msitu wa Mbizi juzi. Alibaini ‘mchezo mchafu’ ulioisababishia halmashauri hiyo hasara hiyo ikiwa ni tozo iliyotakiwa kuilipa baada ya uvunaji na mauzo ya magogo ya msitu huo kufanyika.
Hifadhi ya Msitu wa Mbizi kiko umbali wa kilometa 12 kutoka mjini Sumbawanga ukiwa ni chanzo kikuu cha maji kwa asilimia zaidi ya 80, uko chini ya TFS. Meneja wa Hifadhi ya Msitu wa Mbizi, Mohamed Kihangi alieleza kuwa TFS iliiruhusu Taasisi ya Utafiti wa Misitu nchini (TAFORI) ambayo iliuzia kampuni binafsi ya Daloshebedea General Ltd ya Iringa ambayo ilivuna katika hekta sita za magogo kwenye msitu huo yeye thamani zaidi ya Sh milioni 100.
Kihangi alieleza kuwa aliishirikisha Manispaa katika hatua zote za uvunaji wa msitu huo uliofanyika kwa zaidi ya miezi mitatu huku Manispaa kukana na hawakuwa na taarifa hiyo hadi dakika za mwisho.
Ofisa Misitu wa Manispaa ya Sumbawanga, Joseph Nkonjera awali alikana kushirikishwa katika uvunaji wa magogo katika msitu huo isipokuwa katika hatua za mwisho za uvunaji.
Pia hana taarifa ya ukubwa wa eneo la msitu uliovunwa.
Ndipo Mbunge Hilaly alipombana kwa kumtaka aeleze ukweli kwa kuwa haingii akilini magogo kuweza kusafirishwa kutoka mjini Sumbawanga hadi Iringa bila kuwa na vibali kutoka Ofisi ya Maliasili ya manispaa hiyo.
Nkongera alikiri kuwa alipokea ushuru wa Sh 900,000 kati ya milioni 50 zilizopaswa kulipwa na kampuni ya Dalashebedea General Ltd ya Iringa.
Kutokana na hilo, Mbunge huyo alimtaka Meneja wa Hifadhi ya Misitu ya Mbizi, Kihangi kuwasiliana na TFS , TAFORI na Kampuni ya Daloshebedea kuwasilisha vielelezo vya uvunaji na manunuzi magogo hayo ili waweze kujua ni namna gani manispaa hiyo itapata haki yake kutokana na uvunaji huo.
Pia wamemtaka Ofisa Misitu wa Manispaa hiyo , Nkojera kuwakilisha stakabadhi za manunuzi na malipo ya tozo alizopokea kutoka kampuni binafsi ya Daloshebedea General Ltd.

Chanzo Gazeti la Habari leo

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa