Home » » PADRI,KATEKISTA WAFARIKI AJALINI

PADRI,KATEKISTA WAFARIKI AJALINI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Padri wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mpanda, Matini Kapufi (42 ) na Katekista wa kanisa hilo wa kijiji cha Mtakuja, Parokia ya Inyonga, Patrick Mwendowasaa (60), wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupinduka.
Gari hilo lilipinduka baada ya kuacha njia. Watu wengine wawili walijeruhiwa na wamelazwa hospitali.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alisema ajali hiyo ilitokea jana saa nne asubuhi katika Kijiji cha Kamsisi, Tarafa ya Inyonga, Barabara ya Inyonga kuelekea mkoani Tabora.
Alisema ajali hiyo ililihusisha gari aina ya Toyota Hilux, Pick Up lililokuwa likiendeshwa na Padri Kapufi ambaye ni Paroko wa Parokia ya Mwese, Jimbo Katoliki la Mpanda.
Aliwataja watu waliojeruhiwa kuwa ni Katekista Msaidizi wa Kijiji cha Mtakuja, Parokia ya Inyonga, Daud Saveli (31), ambaye ameumia sehemu za kidevu na mguu wa kushoto na mkazi wa Kijiji cha Mtakuja, Tarafa ya Inyonga, Wilaya ya Mlele, Melikio Maraluma.
Alisema watu hao walipata ajali walipokuwa wakisafiri kutoka Inyonga, Makao Makuu ya Wilaya ya Mlele kwenda Mto Koga, mpakani mwa Mkoa wa Katavi na Tabora kumpokea Askofu Gervas Nyaisonga aliyekuwa akitokea Dodoma baada ya kuhamishiwa Jimbo la Mpanda.
Kamanda Kidavashari alisema baada ya gari hilo kufika Kijiji cha Kamsisi, liliacha njia na kupinduka na kusababisha kifo cha Katekista Mwendowasaa papohapo na Padri Kapufi aliyefariki njiani alipokuwa akipelekwa Kituo cha Afya Inyonga.
Chanzo;Mwananchi
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa