Home » » MWENDESHA BAISKELI AFARIKI KWA KUGONGWA NA GARI

MWENDESHA BAISKELI AFARIKI KWA KUGONGWA NA GARI

Na walter mguluchuma,Sumbawanga



MPANDA baiskeli, Leonard Garimoshi (20), mkazi Kaengesa  wilayani Sumbawanga , mkoa wa Rukwa amefariki dunia  baada ya kugongwa na gari

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa , Jacob Mwaruanda  akitihibitisha  alibainisha tukio  hilo hilo  lilitokea kijijini Katonko , Kata ya Kaengesa  katika  barabara kuu ya Mbeya – Sumbawanga  mkoani hapa ajali ya  basrabarani  iliyohusisha  gari aina ya Toyota Raum  yenye namaba za usajiri T 186 AYJ  lililokuwa likiendeshwa  na Soud Hilal .

Kwa mujibu  Kamanda Mwaruanda  gari  hilo   lilimgonga mwendesha baiskeli huyo  na kufa papo hapo  lilikuwa likitokea Sumbawanga mjini likielekea Jijini Dar Es Salaam.

“Chanzo  cha ajali hii  ya barabarani  ni mwendokasi  wa dereva  wa gari hilo  ambaye  ameshakamatwa na kufikishwa  mahakamani ili  sheria iweze  kuchukua mkondo wake “ alibainisha  .

Katika tukio lingine  Mfanyabishara aitwae Yohana Damian (31) , mkazi  wa eneo  la Jangwani , Manispaa  ya Sumbawanga amevamiwa  na watu  wanne wanaosadikiwa kuwa  vibaka  akiwa dukani kwake  na kuimwibia  vitu mbalibali  nyenye  thamani ya zaidi  ya Sh 800,000.

Kamanda Mwaruanda amethibitisha  kuwa ‘vibaka’  hao  walifanikiwa  kutoroka mara tu  askari polisi walipofika dukani hapo  kwamba jitihada  zinaendelea  kuwabaini  ili  waweze  kufikishwa  kwenye  vyombo vya sheria .


Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa