Home » » UJENZI HOLELA WASHAMIRI SUMBAWANGA

UJENZI HOLELA WASHAMIRI SUMBAWANGA

Mji wa Sumbawanga umekuwa ukipoteza umaridadi wake wa siku za nyuma kutokana na kuzidi kushamiri kwa ujenzi holela unaofanywa na wakazi wa mji huo katika siku za karibuni. Hali hiyo imetajwa kusababishwa na Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga kushindwa kugawa viwanja vipya vya ujenzi kwa muda mrefu kutokana na sababu mbalimbali. Akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani , Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga Bw. William Zackaria Shimwela amesema kuwa tatizo la kutogawiwa kwa viwanja vipya linatokana na Wizara ya Ardhi nyumba na Makazi kushindwa kupitisha kwa ramani mpya za maeneo ambayo tayari yamekwishapimwa kwa takribani miaka mitatu sasa, hivyo wananchi kukata tamaa na kuanza kujengamakazi yao kiholela. Amesema Manispaa yake hivi sasa haina tatizo la wataalamu na hata vifaa ambavyo vinatumika kwaajili ya upimaji ambao wako tayari kufanya kazi muda wote lakini jitihada zao zinakwamishwa na wizara husika. Awali katika kikao hicho katika maswali ya papo kwa papo , Diwani wa kata ya Izia, Bw.Field Kasitu aliuliza Mkurugenzi huyo ni lini Manispaa hiyo itapima maeneo ambayo yamejengwa kiholela ili wananchi waweze kupata hati za nyumba zao wanazozimiliki. Katika swali hilo Mkurugenzi huyo amesisitiza kuwa hawawezi kutoa hati za nyumba kwa wale waliojenga kwenye maeneo yasiyopimwa ilihali akisema kuwa utaratibu unaendelea kwa baadhi ya maeneo hayo kupitiwa na wataalamu wa Idara ya ardhi ili yaweze kupimwa na kuchorwa ramani zake.



Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa