Home » » MWENGE WA UHURU WAMALIZA ZIARA YAKE MKOANI RUKWA LEO, WAPAA ANGANI KWA NDEGE KUENDELEZA MBIO ZAKE MKOANI TABORA

MWENGE WA UHURU WAMALIZA ZIARA YAKE MKOANI RUKWA LEO, WAPAA ANGANI KWA NDEGE KUENDELEZA MBIO ZAKE MKOANI TABORA



Mwenge huo wa Uhuru umetembelea miradi 23 ya maendeleo na miradi 28 ya vikundi Mkoani Rukwa vyenye thamani ya fedha za kitanzania zaidi ya shilingi bilioni 3.4 ikiwa ni mchango wa Serikali kuu, Halmashauri, Wananchi na Wadau wengine wa maendeleo.
Ndege ndogo ya Shirika la hifadhi za Taifa (TANAPA) ikipaa angani katika uwanja wa ndege wa Sumbawanga leo tarehe 23 Julai 2013 ikiwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya, wakimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa sita pamoja na Mwenge wa Uhuru utakaoenda kukabidhiwa Mkoani Tabora na Mkuu huyo wa Mkoa wa Rukwa. Wakimbiza mwenge hao ni Ndugu Juma Ali Simai (Kiongozi), Zamda A. John, Christopher Emmanuel, Seperatus Lubinga, Zuwena Abdallah na Mgeni S. Mgeni.
Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Methew Sedoyyeka akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya Mwenge wa Uhuru mara baada ya kukamilisha ratiba yake katika Wilaya hiyo na Mkoa wa Rukwa kwa ujumla. Mkuu huyo wa Mkoa atasafiri kwa ndege kuukabidhi Mwenge huo Mkoani Tabora.
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akitoa hotuba ya kuwaaga wakimbiza mwenge kitaifa na Mwenge wa Uhuru muda mfupi kabla ya kusafiri na Mwenge huo kwa ajili ya kuukabidhi Mkoani Tabora mapema leo tarehe 23 Julai 2013. Katika hotuba yake hiyo aliwapongeza wakimbiza Mwenge wote na wananchi Mkoani Rukwa kwa kufanikisha zoezi hilo kikamilifu na kuwapa vyeti vya pongezi wakimbiza Mwenge hao wa kitaifa.
 Picha ya pamoja kati ya kikundi cha matarumbeta kilichokuwa mstari wa mbele katika kutumbuiza kwenye ziara ya Mwenge Mkoani Rukwa na baadhi ya wakimbiza Mwenge kitaifa na mratibu wa Mwenge Mkoa wa Rukwa Ndugu Abubakari Serungwe wa kwanza kulia (mbele).
 Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa Ndugu Juma Ali Simai akizungumza na wananchi wa Manispaa ya Sumbawanga katika Stendi kuu ya mabasi Mjini Sumbawanga tarehe 22 Julai 2013. Kulia ni Diwani wa kata ya katandala Ndugu Kisabwite na Mbunge Jimbo la Sumbawanga Mjini Aeshi Hillal.
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Iddi Hassan Kmanta akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Moshi Chang’a Mwenge wa Uhuru mara baada ya kumaliza mbio zake Wilayani humo tarehe 20 Julai 2013.
Mkuu wa Wilaya ya Kalambo machachari katika mbio za mwenge wa Uhuru Moshi Chang’a akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Methew Sedoyyeka Mwenge wa Uhuru mara baada ya kumaliza mbio zake Wilayani Kalambo tarehe 21 Julai 2013
 Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Methwew Sedoyyeka akipokea mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Moshi Chang’a tarehe 21 Julai 2013 na kuahidi kuukimbiza katika wilaya yake kwa amani, nguvu na uadilifu mkubwa.
 Baadhi ya raia wa kigeni nao waliomba kupiga picha na Mwenge wetu wa Uhuru.
Wananchi na wanafunzi walihamasika vya kutosha na Mwenge wa Uhuru kiasi cha wengine kupanda juu ya miti ili waweze kupata taswira yake mwanana.
 Wanafunzi na wananchi wakiwa juu ya miti kushuhudia Mwenge wa Uhuru na ujumbe wake.
 
  Kwa wengine kuuona Mwenge wa Uhuru vizuri haikuwa kazi rahisi walilazimika hata kuhatarisha maisha yao.
 
 Picha ya pamoja kati ya mratibu wa Mwenge Mkoani Rukwa ndugu Abubakar Serungwe na baadhi ya wakimbiza mwenge kitaifa pamoja na katibu wa CCM Sumbawanga Mjini Mama Silaf Maufi.
(Picha na Hamza Temba – Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa “rukwareview.blogspot.com)
t
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa