Home » » RC Manyanya kuwabana maafisa wanaouza maeneo ya wazi

RC Manyanya kuwabana maafisa wanaouza maeneo ya wazi

Mhandisi Stella Manyanya amepanga kuchukua hatua kali za kinidhamu kwa Maafisa ardhi mkoani humo ambao wamekuwa wakiuza maeneo ya wazi yaliyotengwa kwaajili ya shughuli mbalimbali za kijamii.     

Hatua hiyo inafuatia baadhi ya maafisa ardhi hususan katika Manispaa ya Sumbawanga ambao wamekuwa wakilalamikiwa kubadilisha matumizi viwanja vya wazi vilivyotengwa huku wakigubikwa pia na tuhuma rushwa ktk mamlaka zao. 

Akizungumza na chemba ya Wafanyabiasha na Wakulima (TCCIA) mkoani Rukwa, Mh. Manyanya amesema sekta ya viwanda na biashara inashindwa kupiga hatua kwa haraka kutokana na moja ya kikwazo cha wawekezaji wa ndani na nje ya mkoa huo kukosa maeneo ya kuwekeza ambapo yale yaliyotengwa yanavurugwa na baadhi ya maafisa ardhi wenye tamaa ya kupata fedha kwa njia zisizo halali.

Amewatahadharisha wataalamu hao kubadili mienendo yao kwa kuzingia maadili ya kazi zao na kuachana na tamaa ya kuuza maeneo yaliyo wazi.

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa