Home » » WALINZI WA KAMPUNI WASHIKILIWA KWA WIZI WA SH. MILIONI 64 KWA MENEJA WAO‏

WALINZI WA KAMPUNI WASHIKILIWA KWA WIZI WA SH. MILIONI 64 KWA MENEJA WAO‏

Na Walter Mguluchuma
Sumbawanga
POLISI  wilayani  Sumbawanga  mkoani hapa  linamsaka  mlinzi  wa  Export Trading  Company  Ltd  , Jofrey Kabungo (35) akituhumiwa  kuiba  kiasi  cha   Sh,  milioni 64 nyumbani   kwa  Meneja wa  Kampuni  hiyo , Kamlesh Patel (46) .
 Kwa  mujibu   wa Kaimu  Kamanda  wa Polisi  mkoani   Rukwa , Peter Ngusa   Kampuni  hiyo  ya Export Trading Company  Limited yenye  Makao yake  Makuu , Jijini  Dar Es Salaam  inamilikiwa   na Mohamed Dewji .
Akisimulia  kisa  cha  wizi  huo , Ngusa alidai  kuwa  fedha hizo  zilikuwa  zimehifadhiwa  nyumbani  kwa Meneja wa  Kampuni hiyo Patel  chini  ya meza  chumbani  kwake  zikiwa  zimeviringishwa  kwenye kifurushi  kwa ajili  ya  ununuzi  wa ufuta .
Aliongeza kuwa   uchunguzi  wa  awali  umebainisha kuwa   chanzo  cha  tukio  hilo  ni  uzembe  wa  Meneja  wa  Kampuni  hiyo  kwa kuacha kifurushi  ya  fedha  hizo  chini   ya  meza  na kuuacha mlango  ukiwa  wazi .
Kwa mujibu  wa Ngusa ,  mtuhumiwa  huyo alifanikiwa kutoroka   na kujificha  kusikojulikana  mara tu  baada ya  kutenda uhalifu huo ,  licha  ya  kumsaka  lakini  pia Polisi  wanaendelea  na  uchunguzi  wa tukio  hilo .
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa