Home » » RUKWA TENA: MTOTO MWENYE ULIMAVU WA NGOZI "ALBINO" AKATWA MKONO MKOANI RUKWA.

RUKWA TENA: MTOTO MWENYE ULIMAVU WA NGOZI "ALBINO" AKATWA MKONO MKOANI RUKWA.






Na Walter Mguluchuma-Blogs za mikoa
Mpanda


MTOTO wa kiume mwenye  ulemavu  wa ngozi ‘albino” Mwigulu Matomange Magessa  mwenye umri wa miaka  saba  ameshambuliwa  na vijana  watatu  walivaa kininja  na kuunyofoa mkono wake mmoja   na kutokomea  na kusikojulikana .

Kwa mujibu wa Diwani wa Kata  ya Milepa , Apolinari  Macheta tukio hilo lilitokea saa kumi na moja  jioni  wakati  Mwigulu  ambaye  anasoma Darasa la Kwanza  katika Shule  ya Msingi Msia  katika Kata  ya Milepa, Bonde la Ziwa Rukwa  wilayani Sumbawanga  akirejea nyumbani Msia mashambani  akiwa ameongozana na kundi la  wanafunzi  wenzake.

Kwa mujibu wa Diwani , Macheta , mtoto Mwigulu  amelazwa katika zahanati ya Mtowisa  katika Bonde  la Ziwa Rukwa  wilayani Sumbawanga  kwa matibabu  ambapo  hali  yake  inaelezwa kuwa  bado  ni tete  kwani alifikishwa kwenye zahanati hiyo  akiwa  amepoteza fahamu .

Akisimulia  kisa  hicho  cha kusikitisha , Diwani Macheta amedai  kuwa kijiji  cha Msia  kimegawanyika  sehemu mbili “Msia Center”  na “Msia mashambani’ ambapo  mtoto Mwigulu  akiwa  ameongozana  na   kundi  la wanafunzi  wenzie  wakirejea nyumbani ‘Msia Mashambani’  baada ya masomo  ghafla  vijana watatu  wanaodaiwa kuvaa kininja  waliwagutusha  ambapo  mmoja wao anadaiwa  kumkimbiza  Mwingulu  huku wengine wawili  wakiwafukuza  wanafunzi  wengine.

“Licha ya wanafunzi  hao  kupiga kelele  zao  haziweza kusikika  kijijini kwani  walikuwa mbali na makazi  ya watu …… ndipo  yule kijanammoja aliyekuwa  akimfukuza  mtoto ‘albino’ akiwa na  panga aliukata mkono  wake mmoja na kutokomea nao  kusikojulikana “ alisema .

Kwa mujibu wake  watoto  walipofika  kwa wazazi  wa  kule Msia mashambani  waliwasimulia  mkasa  uliowakuta  ndipo  ulipoanza msako  mkali wa kumtafuta mtoto Mwigulu  na kumkuta akiwa  mashamba ni  huku mkono  wake mmoja ukiwa  umenyofolewa  na kumkimbiza  katika zahanati  ya  kijiji  cha jirani  cha Mtowisa ambapo  amelazwa  kwa  matibabu.

Jitihada  za gazeti  hili kumpata  Kaimu Kamanda  wa Polisi Mkoa wa Rukwa,Peter Ngusa  kupitia  simu yake ya mkononi  kwa majaribio  kadhaa  hakuwa na mafanikio  kwani  ilikuwa ikiita bila kupokelewa.

Hata  hivyo  habari za ndani  za  kipolisi  zinathibitisha kutokea  kwa  tukio  hilo  ambapo  hadi sasa  hakuna  yeyote  aliyekamatwa .
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa