Home » » HATARI: ALBINO AVAMIWA NA KUKATWAKATWA NA WATU WASIOJLIKANA KISHA KUONDOKA NA MKONO WAKE WA KUSHOTO‏

HATARI: ALBINO AVAMIWA NA KUKATWAKATWA NA WATU WASIOJLIKANA KISHA KUONDOKA NA MKONO WAKE WA KUSHOTO‏


Na Walter Mguluchuma
Rukwa
WATU wasiofahamika wamevamia nyumba ya mwanamke mwenye ulemavu wa
Ngozi Albino Maria Chambanenje (39) mkazi wa kijiji cha Kavifuti
kilichopo katika wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa na kisha
kumkatakata kwa mapanga na kutoweka na mkono wake wa kushoto.
Hata hivyo tukio hilo la kusikitisha lilitokea wakati mume wa mlemavu
huyo mwenye wake wawili akiwa ameenda kulala nyumba jirani ambayo
ni ya mke mkubwa
Akizungumza mara baada ya kumfikisha mlemavu huyo wa ngozi katika
hospitali ya mkoa wa Rukwa kwa ajili ya matibabu mume wa mlemavu huyo
wa ngozi aitwae Gabriel Yohana ,amesema kuwa tukio hilo la mkewe
kukakwa kwatwa kwa mapanga na kisha watu hao kuondoka na kipande
cha mkono wa kushoto wa mkewe, lilitokea majira ya saa nane usiku
mara baada ya watu hao kuvamia nyumba ya mama huyo huku wakiwa
wamefunga milango ya nyumba za majirani kwa kamba kwa lengo la
kuwazuia majirani hao wasitoe msaada wakati wa tukio hilo.
Bw Yohana amesema kuwa usiku wa kuamikia leo majira ya saa 8 usiku
alifuatwa na mtoto wa kaka yake ambaye alidai kuwa nyumbani kwao
,nyumba ambao analala mama huyo mlemavu wa ngozi kuwa kuna dalili za
watu kukata nyumba kwa kwa panga na kuwa amesikia sauti za watoto wa
mlemavu huyo wa ngozi zililia kwa kuomba msaada.
Aliema kuwa hata hivyo mara baada ya kufika nyumbani hapawalimkuta
mkewe akiwa tayari amekatwa mkuno wake wa kushoto pamoja na kujeruhiwa
sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo kichwani pamoja na mkono wake
wa kulia na ndipo alipoanza kupiga kelele za kuomba msaada na
kugundua ya kuwa nyumba za majirani zimefungwa kwa kamba nje kwa
lengo la kuzuia majirani hao kutoa msaada kwa mama huyo.
Kwa upande wake daktari wa zamu wa hospitali ya mkoa wa Rukwa kitengo
cha tiba za nje Dkt rajabu Lugwashi amekiri kumpokea mama huyo
mwenye ulemavu wa ngozi na kusema kuwa mpaka sasa anaendelea kupatiwa
matibabu ikiwemo kuongezewa damu kutokana na kuvuja damu kwa wingi
mara baada ya tukio hilo.
Amesema kuwa mama huyo aliyekatwa mkono wa kutosho eneo la kiwiko
anaendea kupatiwa matibabu na kuongeza kuwa majeraha yaliyopo katika
maeneo mbalimbali ya kichwa chake aliweza kufikishwa katika kituo cha
afya cha Laela kilichopo umbali kidogo toka katika eneo la tukio na
kushonywa.
Kwa upande wao watendaji wa jeshi la polisi mkoa wa Rukwa walipohojiwa
juu ya tukio hilo walishindwakutoa ushirikiano kwa madai ya kuwa
tukio hilo kuna mtu maalum anayelishugurikia.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa