Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Mhandisi Stella Manyanya, akisoma hotuba ya ufunguzi wa kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa wa Rukwa (RCC) leo mjini Sumbawanga. PIcha zote na Mussa Mwangoka.
Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Desderius Mipata akiwa na Mbunge wa Kwela Ignas Malocha wakifuatilia kwa makini kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa wa Rukwa (RCC) kilichofanyika leo mjini Sumbawanga. Picha na Mussa Mwangoka.
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha ushauri wa mkoa wa Rukwa (RCC) wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa katika kikao hicho kilichofanyika leo mjini Sumbawanga, picha na Mussa Mwangoka.
Mussa Mwangoka, Sumbawanga-Rukwa Yetu
------------------------------------------------
Mussa Mwangoka,Sumbawanga-Rukwa Yetu
MKUU wa Mkoa wa Rukwa, Mhandisi Stella Manyanya amekema tabia ya baadhi ya Wakurugenzi wa halmashauri za Wilaya , Miji na Manispaa mkoani Rukwa kujikopesha fedha za miradi ya maendeleo .
Akizungumza katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Rukwa (RCC) jana Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa kumeibuka tabia kwa baadhi ya Halmashauri kujikopesha fedha za miradi ya maendeleo hivyo kusababisha kuwa na miradi ambayo ni viporo .
Mhandisi Manyanya alisema kuwa Halmashauri ziache mara moja kuibua miradi mipya ya maendeleo kabla ya kuhakikisha viporo vyote vinamalizika na zifanya jitihada kurudisha fedha hizo za miradi mara moja.
Alisema kuwa imebainika kwamba mchezo huo mchafu umekuwa ukifanyika kutokana na Halmashauri kutofanya vikao ambavyo vipo kwa mujibu kwa sheria tabia ambayo nayo inapaswa iachwe mara moja kwani imekuwa ikisababisha kupatikana kwa hati chafu na kushusha mapato ya halmashauri sambamba na ufanisi kwa watumishi wake .
Katika hatua nyingine alisema ili kuepuka na uhitaji mkubwa wa ardhi ni vema makampuni yaliyoonesha nia ya kuwekeza katika kilimo kushirikiana na wakulima kwa maeneo ambayo yanaweza kustawisha mazao wanayoyalenga ambayo ni shayiri na ngano.
Mkuu huyo wa Mkoa aliongeza kuwa kuto washirikisha wananchi imekuwa ni changamoto ambazo wakati mwingine inakwamisha uwekezaji kitu ambacho sio sahihi hivyo mkoa umeliona hilo na unalazimika sasa kuwa na mipango mahususiwa matumizi bora ya ardhi.
Hata hivyo siku za karibuni makampuni makubwa ya kibiashara ya Azam- Bakharesa na Kampuni ya kutengeneza Bia nchini (TBL) yameonesha nia ya kuwekeza katika kilimo cha ngano na shayiri kupitia wakulima wadogo na wale wa kati.
MKUU wa Mkoa wa Rukwa, Mhandisi Stella Manyanya amekema tabia ya baadhi ya Wakurugenzi wa halmashauri za Wilaya , Miji na Manispaa mkoani Rukwa kujikopesha fedha za miradi ya maendeleo .
Akizungumza katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Rukwa (RCC) jana Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa kumeibuka tabia kwa baadhi ya Halmashauri kujikopesha fedha za miradi ya maendeleo hivyo kusababisha kuwa na miradi ambayo ni viporo .
Mhandisi Manyanya alisema kuwa Halmashauri ziache mara moja kuibua miradi mipya ya maendeleo kabla ya kuhakikisha viporo vyote vinamalizika na zifanya jitihada kurudisha fedha hizo za miradi mara moja.
Alisema kuwa imebainika kwamba mchezo huo mchafu umekuwa ukifanyika kutokana na Halmashauri kutofanya vikao ambavyo vipo kwa mujibu kwa sheria tabia ambayo nayo inapaswa iachwe mara moja kwani imekuwa ikisababisha kupatikana kwa hati chafu na kushusha mapato ya halmashauri sambamba na ufanisi kwa watumishi wake .
Katika hatua nyingine alisema ili kuepuka na uhitaji mkubwa wa ardhi ni vema makampuni yaliyoonesha nia ya kuwekeza katika kilimo kushirikiana na wakulima kwa maeneo ambayo yanaweza kustawisha mazao wanayoyalenga ambayo ni shayiri na ngano.
Mkuu huyo wa Mkoa aliongeza kuwa kuto washirikisha wananchi imekuwa ni changamoto ambazo wakati mwingine inakwamisha uwekezaji kitu ambacho sio sahihi hivyo mkoa umeliona hilo na unalazimika sasa kuwa na mipango mahususiwa matumizi bora ya ardhi.
Hata hivyo siku za karibuni makampuni makubwa ya kibiashara ya Azam- Bakharesa na Kampuni ya kutengeneza Bia nchini (TBL) yameonesha nia ya kuwekeza katika kilimo cha ngano na shayiri kupitia wakulima wadogo na wale wa kati.
Blogzamikoa
0 comments:
Post a Comment