Home » » MKUU WA MKOA WA RUKWA AONANA NA UONGOZI WA TBL UNAOTAKA KUWEKEZA KWENYE ZAO LA SHAIRI MKOANI RUKWA

MKUU WA MKOA WA RUKWA AONANA NA UONGOZI WA TBL UNAOTAKA KUWEKEZA KWENYE ZAO LA SHAIRI MKOANI RUKWA



Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza na uongozi wa Kiwanda cha Bia cha Tanzania (TBL) uliomtembelea ofisini kwake leo ukiwa na lengo la kuwekeza kwenye kilimo cha shairi ambayo ni malighafi muhimu katika kiwanda hicho cha kutengeneza bia nchini. Mkoa wa Rukwa una ardhi yenye rutuba kustawisha mazao mbalimbali ya kilimo ikiwemo mchele, mahindi, maharagwe, ngano, alizeti, mtama, ulezi n.k. Katika kuwekeza kwao wataanza kwa kushirikiana na wakulima wadogowadogo ambao wapo Mkoani Rukwa kwa kuwawezesha zana bora za kilimo hicho pamoja na pembejeo ambapo pia watamiliki mashamba yao wenyewe kwa ajili ya kilimo hicho.

Ndugu Gerry Van Den Houten ambaye ni Mkurugenzi wa Usambazaji wa Sabmiller ya South Africa ambayo ina mashirikiano na TBL akielezea lengo na faida za uwekezaji huo ambao licha faida kubwa itakayopatikana pia itatoa ajira kwa vijana wengi Mkoani Rukwa pamoja na kuhamasisha kilimo cha zao hilo. Kulia kwake ni Bennie Basson ambaye ni Menenja wa Shairi wa kiwanda hicho cha bia cha Tanzania (TBL).

Timu ya Uongozi wa TBL ambayo pia ilikuwa imeongozana na baadhi ya wakulima wadogowadogo wa shairi Mkoani Rukwa wakiwa Ofsini kwa Mkuu wa Mkoa huo kwenye mazungumzo juu ya uwekezaji huo.
Picha ya Pamoja kati ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, baadhi ya viongozi wa Mkoa na Viongozi wa TBL uliombatana na baadhi ya wakulima wadogowadogo wa shairi Mkoani Rukwa. 
(Picha na Hamza Temba-Rukwareviw blog-Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa)

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa