Home » » WAKUNGA WA JADI WAPIGWA MARUFUKU RUKWA

WAKUNGA WA JADI WAPIGWA MARUFUKU RUKWA



Mussa Mwangoka, Sumbawanga.(Rukwa yetu Blog)

MGANGA  Mkuu wa Mkoa  wa Rukwa , Dk John Gurisha  amewapiga marufuku  tabia ya wakunga  wa jadi  mkoani  humo  kuzalisha  akinamama  na badala  yake  wawasaidie kuwafikisha  katika  vituo  vinavyotoa  huduma hiyo.

Dk Gurisha alitoa  alisema hayo jana wakati akizungungumza na waandishi  wa habari   ofisini  kwake  mijini   hapa,  ambapo  alisema  wakunga  wa  jadi  wanaweza  kuzalisha  pale  inapotokea  dharura  ambapo  mama   mjamzito  anapopata  uchungu  wa ghafla  lakini  si  vinginevyo.

“ Wakunga  wa jadi  nasema  wasizalishe  akina mama  bali  wawasaidie  kuwafikisha  katika   vituo vya   kutolea  huduma  ili  waweze kupata   huduma  stahiki “  alisema  .

Pia amewapiga marufuku  madaktari  na   matabibu  wanaotoa  huduma  katika  hospitali  na  vituo   vya  afya   vya  umma mkoani  humo  kumwandikia  mgonjwa  dawa  ambayo  haipo  ili  aende kununua  katika  maduka  ya madawa  ya watu   binafsi .

Alisema kuwa  marufuku  hiyo ni  katika  jitihadi  za kuweka  uthibiti  wa madawa  katika  vituo  vya  umma vinavyotoa huduma  ya  afya  mkoani  humo  pia  kuwadhibiti  madaktari  na  matabibu  katika  vituo  hivyo  kufanya  hivyo  ili  wagonjwa walazimike  kununua  dawa katika maduka ya madawa  ya  binafsi  ambayo   baadhi  ya  maduka hayo  yanamilikiwa na  waoa  wenyewe.

Alitahadharisha kuwa  iwapo  itabainika  daktari  ama  tabibu  amekiuka  marufuku  hiyo  basi   atachukuliwa   hatua  kali  ya  kinidhamu  ili  iwe   fundisho  kwa  wengine  wasiige  tabia  hiyo pia alibainisha kuwa Kamati  ya  Manunuzi  ambayo  kwa muda  mrefu ilikuwa  ‘imekufa’  sasa imefufuliwa  upya .

Hata hivyo  alisema kuwa  bado  sekta hiyo  ya  afya mkoani   humo  bado  inakabiliwa na upungufu mkubwa  wa  watumishi  wa  afya  wenye sifa  katika   kada  zote  zikiwemo   za madaktari  bingwa , madaktari , matabibu , wauguzi  na wakunga .
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa