Home » » Mafundi, Vibarua wawafungia Wachina ofisini

Mafundi, Vibarua wawafungia Wachina ofisini


Mussa Mwangoka, Sumbawanga-Rukwa yetu

TAHARUKI  ilitanda  katika  Kambi  ya  Kampuni  ya Ujenzi  ya Kichina  ya kijijini Matai  Wilaya  ya Kalambo   Mkoani  wa Rukwa  baada ya mafundi  na    vibarua  50 walipovamia  kambi  hiyo  na  kuwafungia  ndani “ matajiri  wao” hao wa Kichina  wakishinikiza  kulipwa  posho   na mapunjo  yao ya mishahara.

Vibarua hao wanafanya  kazi  za  ujenzi  katika  Kampuni  ya  Kichina   iitwayo  China Railway  Construction  Ltd  ambayo   inajenga  barabara kutoka   Sumbawanga mjini  kupitia  kijijini  Matai  hadi  Bandari  ya  Kasanga  katika mwambao  mwa Ziwa  Tanganyika  yenye urefu wa kilomita 112  kwa kiwango  cha lami.

Kufuatia   vurugu  hiyo  iliyodumu  kwa  zaidi ya  saa  nne  iliwalazimu  viongozi  wa  kampuni  hiyo  ya  ujenzi  kutoa  taarifa  Kituo  cha  Polisi  cha mjini  Matai ambao  walilazimika   kufika kambini  hapo   na  kutuliza  ghasia  hiyo.

Tukio  hilo  lilitokea  jana  saa  sita  mchana  pale   vibarua  hao wenye hasira   wapatao 53  walipovamia kambi  hiyo  na  kuwafungia  ndani  ‘mabosi’  wao  wa  Kichina  huku wakiwapiga  marufuku  kwenda kujipatia  chakula  cha   mchana.

Kwa mujibu wa  taarifa  hizo  zilizothibitishwa  na Msimamizi  wa  Kampuni  hiyo  Salim Juma  zinaeleza kuwa  ghasia  hizo   zinafuatia  madai  ya  vibarua  hao  yanayotokana na  kupunjwa posho  zao  ambapo  wanadai  kuwa  wamekuwa  wakilipwa  tofauti na  makataba  wao  wa  kazi.

Kwa mujibu  wa madai   ya  vibarua hao  wamedai  kuwa  wamekuwa  wakilipwa  Sh 10,000-  kwa  siku   badala  ya Sh 12,000- kwa mafundi  ilihali  vibarua   wakilipwa  Sh 3,500- kwa siku  badala  ya Sh  5,000-  ambapo  waliaamua  kufunga  lango  kuu  la  kambi  hiyo  na  kuwazuia  wachina  hao kwenda kula   chakula  chao   cha  mchana  hadi   watakapowalipa  posho   na mapunjo yao .

Mkuu  wa  Polisi  wa Wilaya  ya  Kalambo  Hosea  Setieli alithibitisha kutokea  kwa  tukio  hilo  ambapo  aliongeza  kuwa  tayari  askari   polisi  walikuwa  wamepelekwa  katika   eneo la  tukio  ili  kutuliza  ghasia  hizo  na   kuhakikisha  usalama  wa  raia  na  mali  zao .

Hata  hivyo  hakuwa tayari  kueleza  kwa kina   mkasa  huo  kwa kuwa  yeye  alidai   si  msemaji  wa Jeshi  la Polisi .

Hata  hivyo  kwa  kujibu  wa  Salim  hakuna  mtu  yeyote  aliyeumia  wala  uhalibifu  wowote  wa mali  uliotokea  kufuatia ghasia  hizo  ambapo  aliongeza kusema kuwa  Kampuni  ilifikia  makubaliano  ya  kuwalipa  wafanyakazi  hao  leo  asubuhi  ili  kunusuru  ghasia  zaidi   zinazoweza kutokea  na  kuzorotesha  utendaji wa  kazi wa kampuni  hiyo .



Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa