Home » » DC: Moafisa mafisadi wanaitia hasara serikali Sumbawanga

DC: Moafisa mafisadi wanaitia hasara serikali Sumbawanga


Mussa Mwangoka, Sumbawanga-Rukwa yetu

MKUU  wa wilaya  ya  Kalambo  mkoani  Rukwa, Moshi Chang’a  amesema vitendo vya ubinafsi, rushwa na ufisadi kwa  baadhi ya  maofisa Serikalini  kimekuwa  kichochea kikubwa   cha ujenzi holela katika  mijini  hapa nchini jambo ambalo linaloigharimu Serikali kwa kutumia fedha nyingi katika kulipa fidia wananchi wanapotakiwa kuondoka katika maeneo hayo.


Chang’a alisema hayo kwa  nyakati  tofauti  katika  ziara yake iliyoanza juzi  ya kutembelea  Kata  zote  17  zilizopo  wilayani  humo  yenye lengo la kujitambulisha, kukagua  miradi  mbalimbali  ya maendeleo  na kusalimiana na  wananachi.

 Alisema  kuwa  kutokana na  makazi ya  wakazi  wengi  kujengwa  kiholela katika miji   mingi  nchini  Serikali  italazimika kutumia   fedha  nyingi  kuwalipa  fidia  ili  waweze kupisha ujenzi wa huduma muhimu kama barabara, masoko, sehemu za ibada na nyinginezo.

Hivyo,  aliwaagiza  viongozi  wilayani  humo  kuhakikisha wanawashirikisha wadau wote wa maendeleo katika kazi ya upangaji wa mji wa Matai ambayo ni makao makuu ya wilaya hiyo ya Kalambo.
“Kuna uzembe unaofanywa na baadhi ya watendaji Serikalini ambao wamekuwa wakifumbia macho ujenzi holela kwenye baadhi ya miji hapa nchini, hali inayosababisha kuvurugika kwa mipango miji, nitawashughulikia sawasawa” alisema Chang’a.



Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa