Home » » AFUNGWA MIAKA 30 JELA KWA KOSA UNYANG'ANYI WA KUTUMIA SILAHA

AFUNGWA MIAKA 30 JELA KWA KOSA UNYANG'ANYI WA KUTUMIA SILAHA



Mussa Mwangoka, Sumbawanga. Rukwa yetu Blog
 
MAHAKAMA   ya  wilaya ya Sumbawanga  imemuhukumu Nkinga Majeki (35) kutumikia kifungo cha miaka 30 jela  baada ya kumtia  hatiani  kwa kosa  la unyang’anyi  wa  kutumia  silaha ya moto.
Hakimu  wa Mahakama hiyo , Adamu  Mwanjokolo  akisoma  hukumu hiyo  mahakamani  hapo juzi  alisema kuwa  mahakama amemtia hatiani  Majeki  ambaye ni mkazi wa  kijiji cha Mheza  wilayani Chunya  mkoani Mbeya baada ya kuridhishwa  na  ushahidi  wa  upande  wa  mashtaka  pasipo kutia  shaka  yeyote kuwa  mshtakiwa  alitenda kosa hilo .
Kwa mujibu wa  hati  za  mashtaka  zilizowasilishwa mahakamani  hapo  zinaonesha kuwa  upande  wa mashtaka ukiongozwa  na  Mkaguzi Msaidizi wa Polisi , Emanueli Shani uliwaleta mashahidi  watano kutoa  ushahidi  katika shauri hilo.

“Hakika  upande wa mashtaka  umethibitisha  pasipo kuacha shaka yeyote kuwa  mshtakiwa  alitenda kosa hilo  hivyo  natoa  adhabu kali,  ambapo  nakuhukumu  kutumikia kifungo  cha miaka  30   jela  adhabu  ambayo  itakuwa fundisho  sio  tu kwako mshtakiwa  bali  pia kwa wengine  wote  wenye  tabia kama yako  ambayo  inarudisha  nyuma  maendeleo   ya  mtu  binafsi  na  nchi kwa ujumla “alisema akitoa  hukumu  hiyo .

Awali, Upande a mashtaka ulidai  mahakamani  hapo  kuwa mshtakiwa  huyo  alitenda kosa hilo  Novemba 08  mwaka  jana nyakati za usiku  katika  kijiji  cha Kipeta  wilayani  Sumbawanga akiwa na mwenzake  ambaye  hajakamatwa  walipovamia  nyumbani  kwa  Ronald  Lwenje (61)  kijijini humo na kumnyang’anya  fedha taslimu  Sh 5,000,000- baada ya kumtishia  kumpiga  risasi kwa bunduki  waliyokuwa nayo  ambayo haijafahamika  ni  aina  gani  pia haijapatikana.
Kwa mujibu  wa hati   ya  mashtaka  inaonesha kuwa Lwenje  alikuwa  amepokea mafao  yake  siku chache kabla  ya kuvamiwa  baada ya kustaafu kazi  ya ualimu .
Shani  alidai   mahakamani  hapo  kuwa  mshatakiwa alikamatwa  na polisi Novemba , 15 mwaka jana  kijijini  Klyamatundu  wilayani  Sumbawanga  ambapo  alikiri kutenda kosa hilo  alipohojiwa  pia  aliweza kutambuliwa  na  mlalamikaji  wa shauri  hilo.
Mwisho

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa