Home » » NANE WAHOFIWA KUFA MAJI BAADA YA BOTI KUGONGANA

NANE WAHOFIWA KUFA MAJI BAADA YA BOTI KUGONGANA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na   Walter Mguluchuma , Sumbawanga-Rukwa yetu
WATU 8 wanadhaniwa kufa maji katika ziwa Tanganyika baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kutokea kata ya Kirando kwenda Korongwe wilayani Nkasi mkoani Rukwa kugongana na boti ya wavuvi waliokuwa wanakwenda kuvua samaki ambapo boti ya abiria ilipasuka na kuzama majini.

Taarifa iliyotolewa na mkuu wa wilaya Nkasi Idd Hassan Kimanta ilisema kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa tarehe 7 mwezi huu majira ya saa 3 za usiku ambapo baada ya boti hizo kugongana boti la abiria lilizama na boti la wavuvi lililofanya tukio hilo walikimbia hadi boti nyingine iliyokua majini humo ilipokuja kuwakoa.

Alisema baada ya hilo serikali wilayani Nkasi ilichukua hatua za kuanza kuwasaka watu waliodhaniwa kuwa wamekufa maji siku nzima lakini mpaka sasa hakuna mwili wowote wa marehemu uliokutwa majini na kuwa wanasubiri sasa miili hiyo pale itakapoanza kuelea majini na ndipo waokoaji watakapoanza kuiopoa miili hiyo
Alidai kuwa kati ya watu 8 wanaodhaniwa kufa maji kati yao watano ni watu wazima ambapo wanaume ni watatu na wanawake ni wawili,na watoto waliofia katika ziwa hilo ni watatu.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa  wanadhania watu hao kufia majini baada ya ajali hiyo kutokea na wao hawaonekani tena licha ya kuwa miili yao haionekani na ndiyo maana kuna jitihada ambazo serikali inazifanya za kuitafuta miili hiyo yote na kuwa zoezi hilo likikamilika ukweli halisi wa watu waliofia majini utabainika na huenda idadi ikaongezeka zaidi.

Awali afisa mtendaji wa kata ya Korongwe Rock Msalange alimwambia mkuu wa wilaya kuwa baada ya ajali hiyo kutokea na zoezi la kuwakoa abiria waliokuwemo katika boti ya abiria kukamilika waliamua kuwakamata madereva wa boti zote hizo mbili na kuwakabidhi polisi kwa hatua zaidi za kisheria.

Aliwataja madereva wa maboti hayo kuwa ni Stephano Abbas (34) aliyekua akiendesha boti la abiria ikiwa ni pamoja na madereva wawili wa boti la wavuvi ambao ndiyo waliosababisha ajali hiyo ambao ni Approtas Ronati (33) na Gervas Pesambambili (31) ambao bado wanashikiliwa na jeshi la Polisi.

Baadhi ya Wahanga wa tukio hilo walionusurika Korastika Boaz ambaye amempoteza mtoto wake wa kiume wa miaka 6 katika ajali hiyo alisema kuwa ajali hiyo baada ya kutokea yeye alikua na watoto wawili katika boti hiyo na vitu mbalimbali lakini alipatwa na bumbuwazi na kushindwa kumokoa mtoto wake huyo ambaye amefia majini ikiwa ni pamoja na vitu vyake vyote vimepotea katika ziwa hilo

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa