Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akizungumza na madereva wa
Bodaboda na Bajaji wa Manispaa ya Sumbawanga katika uwanja wa Nelson
Mandela.
Baadhi ya Bajaji zikiwa zimepaki katika uwanja ulipofanyikia Mkutano wa madereva wa Bajaji na Bodaboda na Mkuu wa Mkoa.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Rukwa ACP George Kyando akitoa elimu ya
usalama barabarani na kujibu baadhi ya kero zilizotolewa na madereva wa
Bodaboda na bajaji wa Manispaa ya Sumbawanga.
Baadhi ya bodaboda zikiwa zimepaki uwanja wa Nelson Mandela Mjini Sumbawanga.
Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza Kamanda wa Polisi Mkoa
wa Rukwa George Kyando kuwaweka pembeni Mkuu wa Usalama barabarani wa
Wilaya Inspector Suleiman Africanus pamoja na Msaidizi wa Mkuu wa
Usalama barabarani Mkoa Inspector Michael Mwakasungula ili kupisha
uchunguzi kufuatia tuhuma kadhaa zilizoelekezwa dhidi yao.
Agizo hilo amelitoa wakati akijibu kero za madereva wa bajaji na
bodaboda wapatao 4352 kwa mkoa mzima waliowakilishwa na wenzao wa mjini
Sumbawanga baada ya kukutana nao na kusikiliza vilio vyao katika Mkutano
uliofanyika katika Viwanja vya Nelson Mandela mjini Sumbawanga.
Madereva 13 walipata nafasi ya kumuelezea Mh. Wangabo kero wanazopata
wakiwa barabarani huku miongoni mwa kero hizo ambazo ni pamoja na
kupokea rushwa, uonevu usio wa lazima barabarani na kuwaweka mahabusu
kwa visingizio mbalimbali zilielekezwa kwa maafisa hao wa usalama
barabarani.
“Hawa wawili hawa na tuhuma mlizozitoa huenda zina ukweli, RPC nakuagiza
nenda kazichunguze hizi tuhuma zote zilizotolewa hapa kwa kina na
nyinyi muwe mashahidi kwenda polisi kutoa shuhuda zenu, halafu uchukue
hatua stahiki, lakini wakati huo huo unapozichunguza hizi tuhuma wao
uwaweke pembeni, uwape kazi nyingine,”
Amesema
kuwa hakuna mtendaji wa serikali ambaye amepangiwa sehemu akae milele
na milele na kuwa mtumishi asijidanyanye kwamba bila ya yeye kazi za
serikali haziwezi kwenda huku akijitolea mfano kuwa yeye ni Mkuu wa Mkoa
wa 15 tangu kuanzishwa kwa Mkoa huu mwaka 1974, wote walionitangulia
wamepiga kazi wameondoka nae ataondoka.
Aidha,
Mh. Wangabo amewasisitiza madereva hao kusomea sheria za barabarani na
kupata leseni ilikupunguza ajali za barabarani katika Mkoa wa Rukwa huku
akiwapongeza kwa takwimu zinzoonyesha kupungua kwa ajali hizi
ukilinganisha na mwaka 2016.
Katika kulisisitiza hilo Mh. Wangabo alimualika mwalimu wa mafunzo ya
usalama barabarani ili kutoa mafunzo hayo ya siku 3 bure kwa madereva
hao kwa lengo la kutokuwa na ajali katika Mkoa wa Rukwa.huku akimpa
miezi 7 kamanda wa polisi mkoa kuhakikisha bodaboda wote 4352 wanakuwa
na leseni na vitambulisho.
Kwa
upande wake kamanda wa polisi Mkoa ACP George Kyando ameeleza kuwa kwa
ajali za bajaji na bodaboda mwaka 2016 kulikuwa na ajali 18 huku 11
zikisababisha vifo vya watu 20 wakati mwaka 2017 kuemtokea ajali 9 huku 5
zikisababisha vifo vya watu 7.
Yona
Mwangoka ni mmoja wa madereva wa bodaboda aliyedai kuwa na ushahidi wa
video unaoonyesha ukusanyaji wa shilingi 40,000 kuwapa polisi ili
kuachiwa kwa makosa mbalimbali huku risiti zao zikionesha shilingi
30,000, fedha ambazo zilikusanywa na kiongozi wa boda boda baada ya boda
boda hao kukamatwa kwa kosa la kumpiga askari wa usalama barabarani
tukio lililotokea siku mbili kabla ya Mkutano huo.
0 comments:
Post a Comment