Walter Mguluchuma Na Irene Temu
Nkasi
JESHI
la polisi mkoani Rukwa limetoa majina ya watu waliofariki katika ajali
ya Fuso lenye namba za usajili T425 BFF ili ndugu zao wakachukue miili
ya marehemu kwaajili ya kwenda kufanya maziko.
Kamanda
wa polisi mkoani humo Georege Kyando alisema kuwa miili ya watu
waliokufa katikaajali hiyo ni wanawake 10 nawanaume watano huku baadhi
ya ipo katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya wilaya ya
Nkasi.
Aliwataja marehemu hao kuwa ni Domona Tenganamba(41),Emaanuel Rashif(84),Restuta Sunga(35) Salula Revena(38)FeresiaTenganamba(12 )
Prisca Madeni(45).
Aliwataja
wengine kuwa ni mwalimu washuleya msingi Kalambanzite, Richard
Chikwangara(24)Yusta Somambuto(36),Giles Ramadhani(24),
Odetha Madirisha(46)Megi Nalunguli(52)
Kamanda
Kyando Aliwataja wengine kuwa ni Abuu Amani Mandevu(37)Nyandindi
Batrahamu(35) Magdalena Mbalamwezi(50) pamoja na mtoto mwenye umri wa
wiki mbili ambaye bado hajapewa Jina.
Pia
aliwataja majeruhi wa ajali hiyo kuwa ni Dismas Clement(26),Sema
Savery(25)Ally Haruna(33),Yusta Mfundimwa(50)Tenesfory Oscar(36) Amos
Kitambale(25) Neema Mwanandenje(21)Joseph Sungula(28) namwanamke mmoja
ambaye Yupo chumba cha wagonjwa mahututi I. C. U na hajafahamika jina
lake mpaka sasa.
Alisema
kuwa marehemu na majeruhi wa ajari hiyo ni watu kutoka katika mikoa
mbalimbali hapa nchini ni vizuri wananchi wakafuatilia ili kujua kama
kuna ndugu yao wafanye mawasiliano kwani serikali iliahidi kusafirisha
maiti mpaka watakapofanya maziko.
Alisema
kuwa dereva wa gari hilo bado anasakwa na atakapopatikana afikishwe
mbele ya sheria kwa uzembe nakusababisha ajali iliyo sababisha vifo
hivyo.
Naye
mkuu wa wilaya ya Nkasi Said Mtanda alimshukuru rais John Magufuli kwa
kuungana na wafiwa wote katika katika kipindi hiki cha majonzi kwa
kuondokewa na ndugu zao kwa ajali mbaya ya gari.
0 comments:
Post a Comment