Home » » WAWILI KUNYONGWA HADI KUFA KWA KUBAKA KWA ZAMU

WAWILI KUNYONGWA HADI KUFA KWA KUBAKA KWA ZAMU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Imeandikwa na Pety Siyame, Sumbawanga
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga imewahukumu wakazi wawili wa Kijiji cha Kaengesa wilayani Sumbawanga, kifo kwa kunyongwa baada ya kutiwa hatiani kwa kumuua Magreth Lazaro kwa kukusudia baada ya kumbaka kwa zamu.
Washitakiwa hao wawili ni Maurus Simwanza na Edward Chikwema maarufu Jeshi. Walitiwa hatiani kwa kumvamia na kumbaka Magreth kisha wakamshindilia kwa nguvu kitu chenye ncha kali ukeni hadi utumbo wake ukatoka nje na kumsababishia umauti.
Akisoma hukumu hiyo, Jaji wa mahakama hiyo, Dk Adam Mambi alisema wawili hao walitenda kosa hilo kinyume cha Kifungu 199 cha Sheria ya Makosa ya Jinai Sura ya 16, kama ilivyofanyiwa marekebisho 2002.
Alieleza mahakamani hapo marehemu kabla ya kukata roho akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Rukwa, aliwataja washtakiwa hao wawili kwa majina kuwa ndio waliomshambulia na kumuumiza vibaya.
Katika shauri hilo, upande wa mashtaka uliita mashahidi wanne ili kuthibitisha ushahidi wao dhidi ya makosa hayo yaliyokuwa yakiwakabili washtakiwa hao. Awali, Mwendesha Mashtaka , Njoloyota Mwasubira akisaidiana na Safi Kashinde, alidai mahakamani hapo kuwa washtakiwa hao kwa pamoja walitenda uhalifu huo Juni 10 , 2012 saa nne usiku kijiji Kaengesa.
Ilidaiwa kuwa usiku huo wa tukio wawili hao walimvamia binti huyo, aliyekuwa akinywa pombe ya kienyeji katika klabu moja iliyokuwa ikiuza kilevi hicho kijijini humo, ambapo baada ya kutoka nje na kumbaka kwa zamu, walimuingizia kitu chenye ncha kali kwenye sehemu zake za siri hadi utumbo ukatoka nje.
Kwa mujibu wa Njoloyota, mtu huyo kwanza alikimbizwa katika Kituo cha Afya cha Kaengesa kwa matibabu, lakini baadae alipelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Rukwa mjini hapa ambapo alikufa akiwa anapatiwa matibabu.
Upande wa utetezi uliongozwa na Wakili wa Kujitegemea, Peter Kamyalile. Wakati huo huo, mahakama hiyo imemhukumu kifo mkazi wa Kijiji cha Singiwe wilayani Kalambo, Augustino Nandi kwa kunyongwa baada ya kupatikana na hatia ya kumuua kwa makusudi binti yake, Oliveta Nandi (12) kwa wivu wa kimapenzi.
CHANZO HABARI LEO
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa