Home » » WANAUME WAWILI WAHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA BAADA YA KUPATIKANA NA HATIA ZA KUUWA WAKE ZAO

WANAUME WAWILI WAHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA BAADA YA KUPATIKANA NA HATIA ZA KUUWA WAKE ZAO


Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter   Mguluchuma .
     Rukwa yetu Blog
  Mahakama  kuu  ya   Sumbawanga   imewahukumu  watu  wawili  Kunyongwa   hadi  kufa   katika  kesi  mbili  tofauti   baada ya  kupatikana  na  hatia ya kuua   kwa kusudia  wake  zao  huku  mmoja   akipatikana  na  hatia  ya  kumuua  mke  wake  mkubwa  baada ya kumtuhumu kumuua kwa  ushirikina     mke  wake  mkubwa  kuwa  amemuaua   mtoto wake wa  mke  wake  mdogo .
  Hukumu  hiyo  ilitolewa  hapo  jana  na    Jaji wa  Mahakama kuu ya  Sumbawanga  Jaji  Adamu  Mambi  katika  kikao  cha  Mahakama kuu ya  Sumbawanga  kilichofanyika  katika   Mahakama  ya   Wilaya  ya  Mpanda  Mkoa  wa   Katavi .
Katika  kesi ya  kwanza   Mahakama kuu  ilimuhukumu  Shija   Sosoma    Mkazi  wa  Kijiji cha   Mamba   Wilaya ya   Mlele    kunyongwa  hadi  kufa   baada  ya  kupatikana  na hatia  ya   kumuua kwa kusudia  mke wake   mkubwa kwa   kumchinja  baada ya kumtuhumu kuwa ni  mchawi kuwa  alimuua  mtoto  wake wa  mke  wake  mdogo kwa  ushirikina .
 Awali  kwenye  kesi  hiyo  mwendesha  mashitaka   mwanasheria  mkuu wa   Mkoa  wa   Katavi   Achiles   Mulisi   alidai  Mahakamani  hapo kuwa   mshitakiwa   alitenda  kosa  hilo  hapo   hapo   Januari    23 mwaka  2012  huko  katika  Kijiji  cha  Mamba .
  Ilidaiwa  kuwa  siku  hiyo   hiyo    mshitakiwa        Shija   Sosomo     alimchinja  mke  wake  mkubwa   aitwaye   Mwashi   Nkuba    baada ya  kumshutumu  kuwa amemuua  kichawi mtoto wake wa  mke  mdogo .
  Mwendesha  mashita    huyo   alidai  kuwa   mshitakiwa    baada  ya  kufanya  mauwaji  hayo   alikwenda  kutowa  taarifa  kwa   balozi wa nyumba  kumi  na  kumweleza  kuwa  amafanya  mauwaji  ya  kumuua  mke  wake  mkubwa  kwa  kuwa   amemuua   mtoto wake  wa  mke   mdogo .
Katika   kesi  hiyo    mshitakiwa      alikuwa   akitetewa  na   mwanasheria  Elias   Kifunda  ambapo   upande  huo  haukuwa  na   shahidi  yoyote  zaidi ya  mshitakiwa  mwenyewe  huku  upande  wa  mashitaka   ukiwa  na  mashihidi  sita .
Akisoma hukumu  hiyo    Jaji   Adamu     Mambi  aliiambia   Mahakama  kuwa  kutokana  na  ushahidi  uliotolewa  Mahakamani  hapo  Mahakama  pasipo  shaka  yoyote  imeridhika  na ushahidi  uliotolewa na   upande  wa  mashita   hivyo    mshitakiwa  amepatikana    na  hatia   ya  kifungu  cha   sheria  namba 196  na   197  kuua  kwa  kusudia
Hivyo  alitowa  nafasi  kwa   mshitakiwa ya  kujitetea  kabla  haja  somewa  hukumu  hata  hivyo   wakili  Elias  Kifunda   aiieleza  Mahakama  kwa kuwa  mshitakiwa   amepatikana   na hatia  hiyo    ambayo    adhabu  yake  ni  moja tuu kwa  hiyo   Mahakama  itowe  hukumu  kwa   jinsi   sheria  inavyoelekeza .
Nae   Mwanassheria  wa  Serikali   Achiles  Mulisi  aliiomba  mahakama  itowe  adhabu  kali  kwa  mshitakiwa  kwani  mauwaji ya kuuawa  kwa  wanake  yameshamiri  sana  mkoani  Katavi  hivyo  adhabu  kali  ikitolewa  kwa  mshitakiwa   huyo  itakuwa  ni  funzo kwa  watu  wengine.
    Jaji  Adamu   baada ya  kusikiliza  utetezi huo  alisoma hukumu na  kueleza  kuwa   mshitakiwa  mahakama  imemuhukumu   mshitakiwa kwa  kosa   la  kifungo  cha   sheria    Namba   26   ambapo  adhabu  yake  ni  kunyongwa hadi  kufa .
Katika  kesi  nyingine   Mahakama  kuu  ya  Sumbawanga  imemuhukumu  kunyongwa  hadi  kufa   Monde  Ndushi  52   Mkazi  wa   Kijiji  cha   Chamalendi   Tarafa ya   Mpimbwe   Wilaya  ya   Mlele  Kunyongwa  hadi  kufa  baada  ya  kupatikana  na  hatia  ya  kumuua  mke  wake   kwa  makusudi .
  Mwendesha  mashitaka  mwanasheria wa  Serikali  Jamila   Mziray  aliiambia  mahakama  kuwa  mshitakiwa   alitenda  kosa  hilo hapo   Machi  12  mwaka   2016.
Siku  hiyo  ya  tukio   mshitakiwa   alidaiwa  kumuuwa  mke  wake   aitwaye    Ngole   Njile   kwa   kumchoma na   visu  baada  ya   kukasirishwa  na  kitendo  cha  marehemu  kumnyima  mahindi   ndugu  yake .
Mshitakiwa   katika  kesi  hiyo   alitetewa  na  wakili   Elias   Kifunda  ambapo   katika  utetezi  wake    alidai  kuwa  yeye   hakutenda  kosa  hilo na  siku  hiyo ya  tukio  hakuwepo  nyumbani  kwake  bali   alikuwa  amesafiri .
Baada ya  kusikliza  pande  hizo  mbili   Jaji   Adamu Mambi   alitowa  nafasi  kwa  upande wa  utetezi  kuweza   kujitetea  kabla  ya kusomwa kwa  hukumu  ambapo  wakili   Elias   aliiomba   Mahakama   itowe   adhabu  kwa  mujibu  wa   sheria  inavyo  eleza  kwani  kosa  hilo    adhabu  yake  ni  moja .
Mwanasheria  wa  Serikali   Jamila   Mziray   aliiomba   Mahakama  itowe  adhabu  kali  kwa  mshitakiwa  kwani  kitendo  alichokifanya  ni  cha  kikatili  na  pia  amewasababishia   watoto wa  marehemu  kukosa  huduma  za  mama  yao  ambazo  walikuwa  bado wanazihitaji .
Akisoma hukumu  hiyo  Jaji  Adamu    Mambi   aliiambia   Mahakama  kuwa  mshitakiwa   amepatikana  na  hatia ya  kosa  la  kifungu  cha   sheria  namba  196 na  197  hivyo  mahakama  imemuhukumu   Monde   Ndusha  kunyongwa  hadi  kufa .
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa