Home » » WATOTO WAAJIRIWA KWA UJIRA WA NDAMA

WATOTO WAAJIRIWA KWA UJIRA WA NDAMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
BAADHI ya watoto wilayani Nkasi, Rukwa hasa maeneo ya vijijini, wamekuwa wakiajiriwa na familia za wafugaji kwa ujira wa ndama mmoja kwa mwaka.
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi, umebaini watoto hao ambao wengi wao ni wa kabila la Wafipa, wamekuwa wakitumikishwa kazi ya kuchunga ng’ombe na wafugaji wa kabila la Kisukuma.
Mbaya zaidi baadhi ya watoto hao huamua kuacha kabisa masomo na kwenda kufanya kazi hiyo, ambayo mkataba wake huwa ni malipo ya ndama yanayofanywa kati ya familia ya mtoto na mfugaji.
Uchunguzi huo pia umebaini baadhi ya watoto kupata vipigo kutoka kwa wafugaji hao, hasa pale wanapopoteza mifugo wakiwa kazini.
Mmoja wa wakazi wa Kijiji cha Lunyala, nje kidogo ya Mji wa Namanyere wilayani Nkasi, alisema baadhi ya wazazi wanalazimika kuwaingiza watoto wao katika ajira hizo kutokana na ugumu wa maisha.
Ofisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi, Oscar Mdenye, alikiri uwepo wa ajira hizo kwa baadhi ya vijiji, jambo ambalo alisema wanapambana nalo na kuitaka jamii ya maeneo hayo ibadilike na kuacha ukatili huo.
 Chanzo:Tanzania Daima
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa