Home » » NAMNA YA KUSAJILI BIASHARA YOYOTE

NAMNA YA KUSAJILI BIASHARA YOYOTE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Imekuwa ni kawaida kwa watu hapa nchini kufanya biashara bila kufuata taratibu na kanuni za kisheria.
Ni kutokana na kutojali sheria na kanuni, wapo watu ambao hujikuta katika wakati mgumu ikiwa ni pamoja na kufilisiwa biashara zao.
Sababu ya kufilisiwa inaweza kuwa ni kutokana na kuingia mikataba bila kujua taratibu za sheria za kibiashara. Wapo ambao kwa sababu ya kutojua sheria na kanuni za biashara wamekuwa wakiingia kwenye migogoro na Serikali au watu binafsi kimakosa.
Ninachotaka kusema katika safu hii ni kwamba kabla ya kuanzisha biashara yoyote, penda kuifahamu biashara hiyo kisheria; kwa mfano unataka kufanya biashara ya kuuza ngozi ya ng’ombe, kuuza dawa za wanyama au binadamu, sheria zinasemaje hasa?
Ni mambo muhimu sana kuyafahamu. Wapo watu wengi wamekuwa wakisumbuliwa na sheria, sababu kubwa ni wao wenyewe kuanzisha biashara pasipo kuangalia hasa sheria zinasemaje.
Biashara ni nini? Ni shughuli yoyote inayohusisha uuzaji na ununuzi wa vitu au huduma yoyote, kwa lengo la kupata faida. Biashara inaweza kufanywa na mtu binafsi (sole proprietorship), kampuni au kwa kuingia kwenye ubia.
Mfanyabiashara binafsi ni nani? Ni mtu yeyote aliyeamua kuanzisha biashara yoyote akiwa mmiliki pekee ambaye atakuwa ametoa mtaji wake mwenyewe, faida na hasara zote zinakuwa kwake.
Sheria za biashara nchini; Sheria zinazosimamia uanzishaji wa biashara ni zikiwamo zile za usajili wa majina ya biashara (Business names Registration Act Cap 213) na Sheria ya Kodi ya Mapato ( The Income Tax Act). Pia sheria ya Leseni za Biashara Sura ya 208 (The Business Licence Act Cap 208).
Sheria nyingine zinategemeana na aina ya biashara yako mfano, kama ni biashara ya dawa utahitaji kibali cha Taasisi ya Chakula na Dawa (Tanzania Food and Drugs Authority;TFDA).
Nimelazimika kuyatumia haya maneno ya kiingereza kutokana na ukweli kuwa ndiyo tunayokutana nayo tunapokwenda kusajili, kwani Kiingereza kinafahamika nchini kama lugha ya kiofisi.
Utaratibu wa kufuata ili kuanzisha biashara
Ukishakuwa na mtaji pamoja na nia ya kuanzisha biashara, hatua ya kwanza ni kusajili jina la biashara kwa Wakala wa Usajili wa Biashara (BRERA; Business Regulatory and License Agency).
Pili, unatakiwa kuwa na leseni ya biashara ambayo hupatikana katika ofisi za manispaa husika chini ya Sheria ya Leseni ya Biashara Sura ya 208 kifungu cha 3 ambacho kinasema ni marufuku kufanya biashara bila kuwa na leseni halali katika eneo halali.
Tatu unatakiwa kwenda TRA na kupata namba ya mlipa kodi au kwa lugha ya Kiingereza Tax Identification Number (TIN).
Vibali vingine vitatolewa kulingana na shughuli unayotaka kuifanya, kwa mfano kuna biashara zinalazimisha uwe na vibali kutoka Shirika la Viwango la Taifa (TBS), TFDA, Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Baraza la Wakala wa Usalama na Afya mahala pakazi (OSHA) na vinginevyo.
Faida za kuwa mfanyabiashara binafsi
Mfanyabiashara binafsi ana faida nyingi ikiwa ni pamoja na ukweli kwamba hata uanzishaji wake ni rahisi, faida zinakuja moja kwa moja kwa mfanyabishara, kuingiza mshirika mwingine ni rahisi, uanzishaji wake hauna gharama sana, ni rahisi kuibadili na kufuata aina nyingine ya kufanya biashara.
Itaendelea Alhamisi
Jebra Kambole ni mtaalamu wa sheria kutoka Kampuni ya Law Guards Advocates ya Jijini Dar es Salaam.
Chanzo:Mwananchi
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa