Sumbawanga. Polisi mkoani Rukwa inawashikilia
watu wawili akiwemo dereva wa gari mali ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa
Rukwa wakiwa na mizoga miwili ya nyamapori aina ya swala kinyume cha
sheria.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda
amemtaja mmoja wa watuhumiwa hao kuwa ni Innocent Sikazwe “Kajole”
ambapo mtuhumiwa mwingine jina lake halikuweza kufahamika mara moja.
Kwa mujibu wa Mwaruanda, tukio hilo lilitokea juzi
saa saba usiku katika Kijiji cha Nkundi wilayani Nkasi likilihusisha
gari linalodaiwa kuwa mali ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa lililokuwa
likiendeshwa na mtuhumiwa Sikazwe.
Inadaiwa watuhumiwa waliwinda wanyama hao katika shamba la mifugo linalomilikiwa na Dk Chrisant Mzindakaya.
“Dk Mzindakaya alitutaarifu na askari walifika kijijini hapo mara moja na kuwakamata watuhumiwa hao .
“Ndipo tulipowasiliana na maofisa wa wanyamapori
ambao walithibitisha mizoga hiyo miwili ya wanyama hao kuwa ni mali ya
Serikali na watuhumiwa hawakuwa na kibali chochote cha kuwinda wanyama
hao,” alibainisha Mwaruanda .
Alisema walipohojiwa walikiri waliwagonga kwa
bahati mbaya wanyama hao hivyo waliamua kuwapakia kwenye gari hilo. “Hii
ni nyara ya Serikali kama waliwagonga walipaswa kufuata taratibu lakini
haikuwa hivyo,” alisisitiza
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment