Na Walter
Mguluchuma-Sumbawanga
MATUKIO ya mauaji ya kikatili yanayosababishwa na imani za kishirikina mkoani Rukwa yamepungua hadi kufikia visa 30 mwaka jana ukilinganisha na matukio 37 yaliyoripotiwa mwaka 2012.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa , Jacob Mwaruanda kupungua kwa mauaji hayo kunatokana na ushirikiano wa Jeshi la Polisi na wadau wengine wa ulinzi wakiwemo waandishi wa habari na wananchi .
Akifafanua alisema kuwa miongoni mwa makosa ya jinai yaliyogusa sana hisi za wakazi wa mkoani hapa na kwingineko ni pamoja na matukio mawali ambapo watu wenye uelemavu wa ngozi ‘albino walivamiwa na kukatwa mkono moja kila mmoja wao katika matukio tofauti .
“Pia matukio ya wanavijiji vinavvyozunguka mashamba ya Shrika la Ephata wilayani Sumbawanga kuvamia mashamba hayo na kuwapiga walinzi , kuharibu mazao na kuteketeza matrekta kutokana na mgogoro wa ardhi kati yao “ alibainisha .
Kwa mujibu Mwaruanda watuhumiwa wa matukio hayo walikamatwa na mashauri yao yako katika hatua mbalimbali za kutolewa maamuzi mahakamani .
Kwa upande wa usalama barabarani alisema kuwa ajali za barabarani ziliendelea kugharimu maisha ya watu ambapo matukio 37 ya ajali za barabarani zilizotokea mwaka jana zilisababisha vifo 43 ambapo mwaka juzi yaliripotiwa matukio 38 ya ajali za barabarani ambayo yaligharimu maisha ya watu 57
MATUKIO ya mauaji ya kikatili yanayosababishwa na imani za kishirikina mkoani Rukwa yamepungua hadi kufikia visa 30 mwaka jana ukilinganisha na matukio 37 yaliyoripotiwa mwaka 2012.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa , Jacob Mwaruanda kupungua kwa mauaji hayo kunatokana na ushirikiano wa Jeshi la Polisi na wadau wengine wa ulinzi wakiwemo waandishi wa habari na wananchi .
Akifafanua alisema kuwa miongoni mwa makosa ya jinai yaliyogusa sana hisi za wakazi wa mkoani hapa na kwingineko ni pamoja na matukio mawali ambapo watu wenye uelemavu wa ngozi ‘albino walivamiwa na kukatwa mkono moja kila mmoja wao katika matukio tofauti .
“Pia matukio ya wanavijiji vinavvyozunguka mashamba ya Shrika la Ephata wilayani Sumbawanga kuvamia mashamba hayo na kuwapiga walinzi , kuharibu mazao na kuteketeza matrekta kutokana na mgogoro wa ardhi kati yao “ alibainisha .
Kwa mujibu Mwaruanda watuhumiwa wa matukio hayo walikamatwa na mashauri yao yako katika hatua mbalimbali za kutolewa maamuzi mahakamani .
Kwa upande wa usalama barabarani alisema kuwa ajali za barabarani ziliendelea kugharimu maisha ya watu ambapo matukio 37 ya ajali za barabarani zilizotokea mwaka jana zilisababisha vifo 43 ambapo mwaka juzi yaliripotiwa matukio 38 ya ajali za barabarani ambayo yaligharimu maisha ya watu 57
0 comments:
Post a Comment