Home » » Serikali yalaumiwa kuua kilimo

Serikali yalaumiwa kuua kilimo

UONGOZI wa Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA) mkoani Rukwa, umeilaumu serikali kwamba inachangia kuua sekta ya kilimo nchini.
Shutuma hizo zinatokana na serikali kupitia Wakala wa Hifadhi ya Chakula nchini (NFRA) mkoani Rukwa kushindwa kuwalipa wakulima waliowakopesha mahindi kuanzia Agosti hadi sasa na kuishia kutoa ahadi.
Akizungumza na waandishi wa habari mkoani hapa jana, Mwenyekiti wa TCCIA Rukwa, Sadrick Malila ‘Ikuwo’, alisema kitendo cha serikali kushindwa kuwalipa wakulima hao kinazidi kuwaongezea umasikini miongoni mwao.
“Hivi sasa tayari msimu wa kilimo umeshaanza, unadhani mkulima huyo atalimaje ikiwa hana fedha za kununulia pembejeo? Wengi huko vijijini wamebaki kuitazama mvua kwa sababu hawana jeuri ya kuingia shambani,” alisema Ikuwo.
Wakati TCCIA ikisema hivyo, baadhi ya vyama vya siasa mkoani hapa navyo vimelalamikia kitendo cha wakulima kutolipwa fedha wanazodai kutokana na kuuza mahindi NFRA.
Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rukwa, Clemence Bakuli, alisema chama hicho kinaitaka serikali kuwalipa haraka wakulima hao ambao wengi wao wanategemea fedha hizo kwa ajili ya shughuli mbalimbali.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Rukwa, Zeno Nkoswe, alisema kwa hali hiyo mafanikio katika kilimo hayatapatikana kwa kuwa serikali  inavunja moyo wakulima.
Wakulima mkoani Rukwa wanaidai NFRA zaidi ya sh bilioni 10 kutokana na mahindi waliyokopesha mwaka huu.
Chanzo;Tanzania Daima
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa