Home » » LIFAHAMU ZIWA RUKWA AMBALO NDILO ZIWA KUBWA LA MAGADI NCHINI TANZANIA

LIFAHAMU ZIWA RUKWA AMBALO NDILO ZIWA KUBWA LA MAGADI NCHINI TANZANIA



Ziwa Rukwa ni ziwa kubwa la magadi nchini Tanzania. Liko upande wa kusini magharibi ya nchi karibu na Zambia kati ya Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa.
Uenezaji wa ziwa hubadilika mara kwa mara kufuatana na idadi ya mvua inayonyesha katika beseni yake.

Ziwa liko kwa kimo cha mita 800 juu ya UB katika bonde ambalo ni mkono wa Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki. Bonde hili ni sehemu ya kusini ya mkono wa magharibi wa bonde hili na mikono yote miwili inaungana huko Mbeya kabla ya kuendelea kwa pamoja katika Ziwa Nyasa.

Beseni ya ziwa line eneo la takriban 80,000 km². Urefu na upana wake hubadilikabadilika kulingana na kiasi cha mvua inayonyesha. Kati ya mito inayoingia ni mto wa Songwe pekee ulio na maji muda wote. Kuna taarifa ya kwamba ziwa lilipotea wakati mwingine isipokuwa beseni ndogo upande wa kusini Songwe inapoingia hubaki na maji. Kama maji ni mengi ziwa lina urefu wa kilomita 180.

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa