Home » » Wafanyabiashara wahimizwa kununua mashine za TRA

Wafanyabiashara wahimizwa kununua mashine za TRA



MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Rukwa imehimiza ununuzi wa mashine za kutolea stakabadhi ya manunuzi kwa wafanyabiashara wa kati  kwa kuwa zina manufaa kwa mfanyabiashara, pia zitachangia kuongeza makusanyo ya kodi.
Meneja wa TRA  Rukwa, Philipo Kimune, alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu uzinduzi wa Wiki ya Mlipa Kodi itakayofikia kilele Novemba 8, mwaka huu.
Meneja Kimune alisema lengo ni kuhakikisha wafanyabiashara 2,213 waliopo Rukwa wananunua mashine hizo ambapo hadi sasa tayari wafanyabiashara 100 wamenunua.
Meneja huyo alikiri kwamba pamoja na gharama kubwa ya kununua mashine inayouzwa sh 800,000 lakini serikali kupitia mamlaka hiyo imeweka utaratibu mzuri wa kurudisha fedha hizo kwa wafanyabiashara mara tu baada ya kutengeneza hesabu za mwaka.
Kwa mujibu wa Kimune, Wiki ya Mlipa Kodi mwaka huu inaadhimishwa kwa kufanyika shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa msaada hospitalini, kituo cha watoto yatima cha Bethania na Gereza la Rukwa.
 CHANZO;TANZANIA DAIMA
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa