Home » » WAANDISHI WA HABARI WAGOMA KUANDIKA HABARI ZA MKUU WA MKOA RUKWA

WAANDISHI WA HABARI WAGOMA KUANDIKA HABARI ZA MKUU WA MKOA RUKWA

UONGOZI wa Klabu ya waandishi wa habari mkoani Rukwa (RKPC), umewazuia wanachama wake ambao ni waandishi wa habari kuacha mara moja kuandika na kutangaza taarifa zozote zinazomhusu Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Stella Manyanya kwa madai ya kutoa kauli za kuwadhalilisha waandishi wa habari wa mkoa huo
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Klabu  hiyo ya waandishi wa habari mkoani humo , Peti Siyame  alisema jana kuwa uamuzi  huo ulifikiwa katika kikao  cha dharura  cha Kamati ya Utendaji ya Klabu hiyo.

Ambapo kikao hicho pamoja na mambo mengine kilipokea taarifa ya kile kilichojili kwenye kikao cha kamati ya ushauri wa mkoa wa Rukwa (Rcc) ambapo kiongozi huyo wa Serikali inadawa kutoa lugha zisizopendeza kwa waandishi hao. 
" Maamuzi hayo  yalifikiwa Septemba  28 mwaka  huu  katika  kikoa  cha dharura  cha Kamati  ya Utendaji ya Rukwa Press Klabu baada ya kujadili kwa kina kauli ya maudhi, kejeli, dharau, udhalilishaji na unyanyasaji dhidi ya waandishi mbele ya wajumbe wa Rcc zaidi ya 70 kwenye kikao kilichofanyika mjini Laela wilayani Sumbawanga" alisema Siyame.
Siyame pasipo kufafanua kuali hiyo zilizowakera waandishi hao lakini alidai kuwa rungu hilo pia limemwangukia katibu tawala wa mkoa wa Rukwa Salum Chima ambaye amekuwa hana mahusiano mazuri na waandishi kwa muda mrefu sasa.
Amesisitiza kwa mahusiano hayo yatarejea tu baada ya mkuu huyo wa mkoa na msaidizi wake watakawaomba radhi waandishi kwenye kikao kijacho cha kamati ya ushauri ya mkoa (RCC) kwani ndio alikozungumza lugha zisizo sahihi dhidi ya wanahabari hao.
"Sisi tuliamini kwamba mkuu wa mkoa hakutumia busara kabisa.....alipaswa atuite pembeni kama kuna tatizo na kutueleza sio kuzungumza kwenye hadhara ya watu....wengine ni wadau wetu wakubwa tunaheshimiana wanajua mchango wetu kwenye maendeleo ya mkoa huu, ndio maana alivyoongea wengine waliguna na kucheka.
Alienda mbali zaidi na kueleza kuwa kufanya kazi za kutangaza mkoa sio kumwandika yeye binafsi, sasa yeye anataka aandikwe yeye tu ndio ionekane unatangaza mkoa....kamwe hatuwezi kufanya hivyo, tutafanya kazi kwa maslahi ya umma sio yeye" aliongeza Mwenyekiti huyo 
Manyanya tayari ameanza kuonja chungu ya waandishi kutofanya nae kazi baada ya juzi waandishi kuondoka wakati akipanda jukwaani katika hafla fupi ya kukabidhi nyumba 20 zilizojengwa na Taasisi ya Mkapa Foundation kwa watumishi wa afya iliyofanyika kwenye kijiji cha Chipu.
Pia wanahabari hao juzi walikataa mwaliko wake wakati makamu wa kwanza Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Maalim Seif Shariif Hamad, alipokuwa mkoani Rukwa kwa ajili ya kufunga Sherehe za kiislamu za Hija ndogo (Jitimai).
Mgogoro wa waandishi hao na viongozi wa Serikali ni wa pili baada ya mwaka 2007 walitangaza kuvunja uhusiano wa kikazi na aliyekuwa kamanda wa Polisi mkoa wa Rukwa Germanus Mpongoliana baada ya kuwazuia kufanya kazi wakati wa ujio wa Mkuu wa jeshi la polisi Nchini Said Mwema.
Busara za umoja wa Klabu za waandishi wa habari nchini (UTPC), Baraza la Habari na Mwema mwenyewe ndio zilizorudisha mahusiano kati ya waandishi na Kamanda huyo.

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa