Home » » Maafisa afya Rukwa kuchukuliwa hatua za kinidhamu

Maafisa afya Rukwa kuchukuliwa hatua za kinidhamu

Serikali mkoani Rukwa imesema upo umuhimu wa kuanza kutekeleza mpango wa kuwachukulia hatua za kisheria na za kinidhamu maafisa afya wa mkoa huo watakaobainika kuzembea katika kusimamia suala la usafi wa mazingira katika maeneo yao lengo ikiwa ni kuzuia magonjwa ya mlipuko ya mara kwa mara.

Akizungumza na wadau wa afya katika kikao kilichowashirikisha pia wakuu wa wilaya pamoja na viongozi wengine watendaji wa mkoa wa Rukwa,mkuu wa mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya amesema kuwa utaratibu huo utakwenda pamoja na kuwafukuza kazi maafisa afya watakaobainika kushindwa kutimiza majikumu yao ipasavyo.
Hata hivyo mkuu huyo wa mkoa wa Rukwa amelazimika kutoa msimamo huo mkali kufuatia kusuasua kwa kampeni ya usafi wa mazingira ijulikanayo kwa jina la sumbawanga ngara iliyozinduliwa mapema mwaka jana na makamu wa rais iliyolenga kuwa na mikakati endelevu ya kusimamia usafi wa mazingira.

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa