Katibu Mtendaji wa muungano wa asasi zisizo za Kiserikali mkoani Rukwa, Stanley Mshana akitoa mada jana kwenye mdahalo wa kuelimisha wananchi wa kijiji cha Mwazye kuhusu mabadiliko ya Tabianchi. Picha na Mussa Mwangoka.
Baadhi wa wakazi wa kijiji cha Mwazye wakifuatilia kwa makini mdahalo kuhusu mabadiliko ya tabianchi uliofanyika kwenye ofisi za kata ya Mwazye jana. picha na Mussa Mwangoka.
Mjumbe wa bodi ya muungano wa asasi zisizo za Kiserikali mkoani Rukwa, Josepha Michese akitoa mada jana kwenye mdahalo wa kuelimisha wananchi wa kijiji cha Mwazye kuhusu mabadiliko ya Tabianchi. Picha na Mussa Mwangoka.
Mussa Mwangoka, Sumbawanga-Rukwa Yetu.
WANANCHI wa Mkoa wa Rukwa, wametakiwa kuacha kuharibu mazingira ili waweze kuepukana na athari kubwa ya mabadiliko ya tabia nchi kama ilivyo katika nchi nyingi za magharibi.
Katibu Mtendaji wa muungano wa Asasi zisizo za Kiserikali Mkoani Rukwa (Rango), Stanley Mshana alitoa tahadhari hiyo jana kwa wananchi wa kijiji cha Mwazye kata ya Mwimbi wilayani Kalambo, wakati akitoa mada kwenye mdahalo wa kuelimisha wananchi kuhusu mabadiliko ya Tabianchi uliofadhiliwa na shirika la Civil Society for Foundation.
Alisema kuwa mabadiliko ya tabia nchi yanayotokea hivi sasa nchini ni matokeo ya uharibifu wa mazingira, ambapo baadhi ya wananchi wamekuwa wakilima katika vyanzo vya maji, ukataji wa miti na uchomaji ovyo wa misitu.
Alisema kutokana na hali hiyo baadhi ya maeneo yamekuwa na ukame, joto limeongezeka ukilinganisha na miaka ya nyuma, kitu ambacho kamwe hakiwezi kufumbiwa macho hivyo ni wajibu wa wananchi kuchukua tahadhari na kuacha kuharibu mazingira.
Alisema kuwa ili kuhakisha wanadhibiti hali ya uhalibifu wa mazingira katika maeneo yao hawana budi kupanda miti na kutoruhusu ukataji holela na uchomaji moto ovyo wa misitu kama ilivyo hivi sasa.
Naye Mjumbe wa bodi ya Asasi hiyo, Josephat Michese, alisema licha ya mkoa wa Rukwa ambako athari za mabadiliko ya tabia nchi si kubwa sana lakini katika baadhi ya mikoa zimeanza kuonekana ambapo ugonjwa wa malaria umeenea kwa kasi kwenye maeneo ambayo haukuwa wa kawaida kama vile Amani (Tanga), Mpwapwa, Lushoto, Rungwe, Njombe, Mufindi na Muleba kutokana na mabadiliko ya jotobaridi.
Alisema kuwa Wilaya ya Hanang na Babati zimepata milipuko ya Malaria kutokana na ukame ambao pia umesababisha utapiamlo na upungufu wa kinga na uwezo wa kuhimili magonjwa kitu ambacho si kizuri kutokea katika mkoa wa Rukwa hivyo wananchi wanatakiwa kuchukua tahadhari kabla hali kama hiyo haijatokea.
Blogzamikoa
WANANCHI wa Mkoa wa Rukwa, wametakiwa kuacha kuharibu mazingira ili waweze kuepukana na athari kubwa ya mabadiliko ya tabia nchi kama ilivyo katika nchi nyingi za magharibi.
Katibu Mtendaji wa muungano wa Asasi zisizo za Kiserikali Mkoani Rukwa (Rango), Stanley Mshana alitoa tahadhari hiyo jana kwa wananchi wa kijiji cha Mwazye kata ya Mwimbi wilayani Kalambo, wakati akitoa mada kwenye mdahalo wa kuelimisha wananchi kuhusu mabadiliko ya Tabianchi uliofadhiliwa na shirika la Civil Society for Foundation.
Alisema kuwa mabadiliko ya tabia nchi yanayotokea hivi sasa nchini ni matokeo ya uharibifu wa mazingira, ambapo baadhi ya wananchi wamekuwa wakilima katika vyanzo vya maji, ukataji wa miti na uchomaji ovyo wa misitu.
Alisema kutokana na hali hiyo baadhi ya maeneo yamekuwa na ukame, joto limeongezeka ukilinganisha na miaka ya nyuma, kitu ambacho kamwe hakiwezi kufumbiwa macho hivyo ni wajibu wa wananchi kuchukua tahadhari na kuacha kuharibu mazingira.
Alisema kuwa ili kuhakisha wanadhibiti hali ya uhalibifu wa mazingira katika maeneo yao hawana budi kupanda miti na kutoruhusu ukataji holela na uchomaji moto ovyo wa misitu kama ilivyo hivi sasa.
Naye Mjumbe wa bodi ya Asasi hiyo, Josephat Michese, alisema licha ya mkoa wa Rukwa ambako athari za mabadiliko ya tabia nchi si kubwa sana lakini katika baadhi ya mikoa zimeanza kuonekana ambapo ugonjwa wa malaria umeenea kwa kasi kwenye maeneo ambayo haukuwa wa kawaida kama vile Amani (Tanga), Mpwapwa, Lushoto, Rungwe, Njombe, Mufindi na Muleba kutokana na mabadiliko ya jotobaridi.
Alisema kuwa Wilaya ya Hanang na Babati zimepata milipuko ya Malaria kutokana na ukame ambao pia umesababisha utapiamlo na upungufu wa kinga na uwezo wa kuhimili magonjwa kitu ambacho si kizuri kutokea katika mkoa wa Rukwa hivyo wananchi wanatakiwa kuchukua tahadhari kabla hali kama hiyo haijatokea.
Blogzamikoa
0 comments:
Post a Comment