Home » » Majambazi kutoka nchi jirani yatishia maisha ya wakazi Ziwa Tanganyika

Majambazi kutoka nchi jirani yatishia maisha ya wakazi Ziwa Tanganyika


Mussa Mwangoka, Sumbawanga.

IMEELEZWA kuwa maisha ya wakazi wa mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Nkasi mkoani Rukwa yako hatarini kwa  kukumbwa na matukio ya mara kwa mara ya kuvamiwa na Majambazi toka nchi jirani  kutokana na kukosekana  kwa mawasiliana na vituo vya polisi  vilivyo  katika maeneo hayo.

Mkuu wa wa wilaya ya Nkasi, Iddy  Kimanta, alisema hayo juzi  wakati akizungumza na uongozi wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Rukwa waliofanya ziara ya siku mbili kukagua shughuli za maendeleo kwenye  wilaya hiyo.

Kimanta alisema kuwa kutokana na kukosekana kwa mawasiliano, majambazi hao kutoka nchi jirani wamekuwa wakipata mwanya wa kufanya vitendo vya kihalifu huku wakifahamu kuwa itachukua muda mrefu vyombo vya usalama kufika kwenye maeneo hayo.

Alisema kuwa hali hiyo imewafanya wakazi wa maeneo hayo kuishi kwa hofu kubwa kwa kudhani kuwa wanaweza kuvamiwa wakati wowote hali inayochangia kudumua kwa uchumi wa wananchi hao.

Mkuu  huyo wa wilaya alisema katika kukabiliana  na hali hiyo wilaya imeanza kuwahamasisha wakazi wa maeneo hayo kujenga vituo vya polisi, lakini pia kuzishawishi kampuni za simu za mikononni kufikiria kujenga minara ya mawasiliano kwenye maeneo hayo ambayo yana mwingiliano mkubwa watu na shughuli nyingi za kiuchumi.

Maeneo ya mwambao mwa Ziwa Tanganyika hususani kwenye kata za Kala na Wampembe wilayani Nkasi yamekuwa yakikumbwa na uvamizi wa mara kwa mara ambapo Majambazi toka nchi jirani kwa kushirikana na baadhi ya wenyeji wamekuwa wakivamia na kuwapora wavuvi na baadhi ya Wafanyabiashara kisha kutoroka kwa mitumbwi kwenda nchi jirani.

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa