Home » » Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Chikawe awataka wanafunzi kujiandisha kupiga kura Oktoba.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Chikawe awataka wanafunzi kujiandisha kupiga kura Oktoba.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe, amewataka wanafunzi wa kidato cha sita kujitokeza kwa wingi na kupiga kura katika uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu, ili kumchagua kiongozi atakayewafaa.
 
Chikawe alitoa ushauri huo kwenye mahafali ya nne ya kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya St. Cathedral.
 
Chikawe alisema watakapojiandikisha katika daftari la kudumu la wapigakura, itawasaidia kumpigia kura kiongozi wanayemtaka.
 
“Usipojiandikisha kupiga kura utaishia kulalamika kuwa kiongozi huyu hafai, ila ukijitokeza kwenye uchaguzi na kupiga kura, utamchagua kiongozi unayemtaka na atakaye kufaa,” alisema Chikawe.
 
Pia, aliwataka wahitimu hao kujiepusha makundi ya kihalifu ukiwamo ugaidi ambayo yanaweza kuchafua sifa zao.
 
“Dunia inakabiliwa na changamoto mbalimbali za kigaidi, naomba msijihusishe wala kushiriki katika vitendo hivyo ambavyo vinaweza kuwaingiza kwenye makundi yasiyofaa na kuharibu sifa zenu,” alisema.
 
Naye Mkuu wa shule hiyo, Sister Theodora Faustine,  alimshukuru Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, kwa kuwasiadia kuwapa shule hiyo.
SOURCE: NIPASHE

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa