Home » » NFRA YASHINDWA KULIPA MILIONI 600

NFRA YASHINDWA KULIPA MILIONI 600

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
WAKALA wa Akiba ya Chakula wa Taifa (NFRA), ameshindwa kulipa deni la zaidi ya sh. milioni 600 zinazodaiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa kutoka kwenye ushuru wa mahindi ya wakulima kwa misimu mitatu mfululizo.
Hali hiyo imeiweka katika kipindi kigumu halmashauri ya Nkasi kwa kuikosesha mapato ya ndani yanayofikia asilimia 30 kutoka kwenye zao la mahindi na hivyo kukwamishwa utekelezaji wa maendeleo ya jamii.
Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Kimulika Galikunga alieleza hayo juzi wakati akihojiwa na Tanzania Daima kuhusu madai yanayotolewa na wananchi juu ya mkwamo wa utekelezaji wa miradi.
Alisema kuwa licha ya kuwepo kwa changamoto nyingi za ukusanyaji wa mapato ya ndani bado mdai wao mkubwa ni NFRA, anayedaiwa sh. 629,561,077.
Galikunga alisema kuwa miaka mitatu mfululizo wakala huyo amekuwa akinunua mazao ya wakulima lakini hajalipa ushuru wa mazao aliyonunua na kusababisha deni hilo kuongezeka zaidi.
Akifafanua juu ya deni hilo, alisema katika msimu wa 2010/2011, NFRA ilikuwa na deni la sh.103,668,990 na mwaka 2011/2012 deni lilikuwa sh. 410,333087, ambapo alilipa sh. milioni 200 akabakiza deni la sh. 210,333,087.
Alisema kuwa deni hilo liliongezeka tena msimu wa kilimo mwaka 2012/2013 na kuwa sh. 315,559,000, hivyo kufanya jumla kwa misimu yote mitatu kufikia sh. 629,561,077.
Kwa mujibu wa mkurugenzi, jitihada mbalimbali za ufuatiliaji wa madai ya hayo zimekuwa zikifanywa pia na Katibu Tawala wa mkoa wa Rukwa na timu ya maafisa wa halmashauri hiyo kwenda jijini Dar es Salaam lakini hakuna matunda yaliyoonekana zaidi ya kuendelea kupigwa danadana. 
Chanzo;Tanzania Daima 
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa