Home » » DR CHRISTIAN MZINDAKAYA ANYANG'ANYWA NYUMBA 12 ZA UMMA AMBAZO ALIKUWA AMEZIPANGA KIBIASHARA KWA MIAKA 12.

DR CHRISTIAN MZINDAKAYA ANYANG'ANYWA NYUMBA 12 ZA UMMA AMBAZO ALIKUWA AMEZIPANGA KIBIASHARA KWA MIAKA 12.



Jiunge na Huduma ya Tone Mobile News Bure kabisa kupitia Whatsapp yako na uwe wa kwanza kupata kile kinachotokea ni Rahisi sana Ingia katika uwanja wa kuandika ujumbe mfupi wa maneno katika Whatsapp yako kisha andika TONE MOBILE NEWS tuma kwenye namba 0756364660 utapokea ujumbe kuwa umeunganishwa. 




 Walter  Mguluchuma Sumbawanga .- Rukwa yetu

HATIMAYE wizara ya Ujenzi  imeinyang’anya Kampuni ya Agriculture and Animal Food Industries Ltd (SAAFI) iliyomilikiwa na mwekezaji mzalendo,na mwanasiasa mkongwe , Dk  Chrisant Mzindakaya  nyumba 12 za umma Serikali ambazo alikuwaamezipanga  kibiashara  kwa miaka 12 .

Nyumba hizo ambapo 11 za kuishi   na moja  ikiwa ni ofisi  zilijengwa na  Shirika la Maendeleo la  nchini Norway  mwaka  1988  zimekabidhiwa rasmi Juni 17 , mwaka huu,  kwa Wakala  wa Majengo (TBA)  mkoani  hapa  na Wizara ya Ujenzi .

Akizungumza  na waandishi wa habari  kuhusu   uamuzi  huo wa Serikali  baada ya kukagua  nyumba hizo  jana , Mbunge  wa Sumbawanga Mjini  (CCM), Aish Hilaly  alisema :- “ Leo  nina  furaha kubwa  sana  kwani  nyumba hizi  zilikuwa  zikininyima usingizi kutokana  na  maofisa serikalini  wakimwemo  majaji  na baadhi ya wakuu  wa idara   kuishi katika  nyumba za kupanga  lakini  sasa  wataishi katika nyumba  hizi  ambazo ni bora  zenye  ulinzi  mzuri  na usalama  wa  kutosha “ alibainisha .

Nyumba maarufu kama ‘compound ‘ limejengwa  katika  eneo  la Mkoani  katika Mji  wa Sumbawanga .

Alibainisha kuwa  baada ya kutembelea  nyumba  hizo na kuzikagua  akiongozana  na Meneja wa Wakala wa Majengo  mkoa wa Rukwa , Deocles Kalikawe amebaini kuwepo  kwa mapungufu makubwa  akidai  kuwa mwekezaji  aliyezipanga kibiashara  atalipia gharama zote za ukarabati .

“Nampongeza  Waziri wa Ujenzi , Dr John Pombe Magufuli  kwa  maamuzi  magumu aliyoyafanya  ya kuzirejesha  nyumba hizi  Serikalini  kupitia TAB…… nimemshauri Meneja  wa TBA mkoani hapa  moja ya  nyumba hizi  iwe  kwa ajili ya kufikia  viongozi  wa kitaifa  kwani  iliweahi kutokea  tulifikiwa na wageni wawili  kutoka taifani mmoja  alilala Ikulu  ndogo  lakini mwingine  alilazimika  kulala  hotelini “ alisisitiza

Nae Meneja wa TBA mkoani hapa , Kalikawe  alieleza  kuwa  mara  baada ya kukabidhiwa rasmi  nyumba  hizo  waliwamua kuweka walinzi  wao  wakati  wakijipanga  kufanya  tathmini ya  ukarabati wa  nyumba  hizo  ili ziweze  kupangishwa  kwa  majaji  na watumishi wa mahakama  pia  wakuu  wa idara  .

Alibainisha kuwa  kati ya nyumba hizo tatu  ni za daraja A zenye  vyumba vitano , tatu zingine  nazo ni daraja A  lakini zina vyumba  vinne  na  nyumba tano  daraja B  zikiwa na  vyumba  viwili .

Wakazi  wa mjini hapa  waliohojiwa na  mwandishi  wa habari  hizi  wameipongeza Serikali  kwa  kuchukua uamuzi huo  kwamba  utapunguza tatizo  la  uhaba  wa nyumba kwa  maofisa Serikalini .

“Tatizo la uhaba  wa nyumba ni  changamoto  kubwa sana  mkoani hapa  ambapo  imesababisha  baadhi ya  watumishi  wanaopangiwa  kuja kufanya kazi  huku  kukataa  kuja  kuripoti  au wanafika na kuripoti lakini  wakiondoka  hawarfudi  tena …” anasema  Enos Budodi mkazi  wa mjini hapa .

Nae Mkurugenzi   wa Asasi isiyo  ya Kiserikali inayojishughulisha na  shughuli za kijamii  na maendeleo (UDESO kwa mikoa ya Rukwa na Katavi, Eden Wayimba  alieleza kuwa  kurejeshwa Serikali kujireshea mali yake  yenyewe  kutawapunguzia  gharama  za maisha watumishi wa umma  watakaopangishwa .

Kurejeshwa kwa nyumba hizo, ni ushindi mkubwa kwa Aeshi ambaye tangu awali amekuwa hana mahusiano mazuri ya kisiasa na Dk. Mzindakaya ambapo mara kadhaa mbunge huyo alikuwa akihoji uhalali ya nyumba hizo kumilikiwa na kampuni ya mtu binafsi badala ya kutumia na watumishi wa Serikali.

Lakini wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanadai kwa uamuzi huo utaongeza chuki ya kisiasa kati ya wanasiasa hao wawili mahasimu ambao mara ya mwisho walikutana mwezi meikwenye ibada ya kusimikwa kwa askofu wa  kanisa Moravian jimbo la Rukwa, Cornad Nguvumali.

Ibada hiyo ilifanyika kwenye uwanja wa michezo wa Nelson Mandela uliopo mjini hapa ambapo mkuu wa mkoa aliwataka wazike tofauti zao lakini Dk. Mzindakaya alikataa kumsamehe Aeshi kwa madai hakuandaliwa kiroho kutoa msahama kwenye ibada hiyo.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa