Home » » Mwalimu aliyefumaniwa akajeruhi atwangwa faini

Mwalimu aliyefumaniwa akajeruhi atwangwa faini

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

MWALIMU wa Shule ya Msingi Katani, Lingston Nelson (36) amelipa faini ya Sh 400,000 baada ya kujeruhi kwa panga na msumeno katika tukio la kufumaniwa na mke wa mtu. Mwalimu huyo ametiwa hatiani na Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Nkasi, mkoani Rukwa, Ramadhan Mgamalila.
Akitoa hukumu hiyo hakimu Mgamalila alisema ameridhika na ushahidi uliotolewa upande wa mashtaka ambao uliongozwa na Mwendesha Mashtaka, Hamimu Gwelo.
Aidha katika kesi hiyo, mtuhumiwa mwingine Betha Sangu (31) mkazi wa kijiji cha Katani wilayani Nkasi ambaye alishtakiwa na Lingston kwa kosa la kujeruhi, aliachiwa huru na mahakama hiyo baada ya kukosekana kwa ushahidi wa kutosha kumhusisha na kadhia hiyo ya kujeruhi.
Betha ndiye aliyekuwa na Lingston siku ya fumanizi. Hakimu Mgamalila alimtaka Lingston kulipa Sh 400,000 kati ya hizo, Sh 100,000 ikiwa ni faini ya ugoni na Sh 300,000 ikiwa ni fidia kwa majeruhi hao wawili ambapo kila mmoja wao atalipwa Sh 150,000. Mshtakiwa alilipa kiasi hicho cha fedha na kuachiwa huru.
Akisoma hukumu hiyo juzi, Mgamalila aliieleza mahakama hiyo kuwa Oktoba 10, mwaka jana saa tatu usiku kijijini Katani mshtakiwa Lingston alikuwa akifanya mapenzi na Beatha ambaye ni mke wa kwanza wa Richard Sarungi (33) mkazi wa kijijini humo.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa usiku huo wa tukio, Richard ambaye alikuwa nyumbani kwa mkewe mdogo kijijini humo alipewa taarifa kuwa mkewe alikuwa akifanya mapenzi na mwanaume mwingine nyumbani kwake mwanamke huyo.
Kwa mujibu wa hati hiyo ya mashtaka, Richard akifuatana na mdogo wake aitwae Stanislaus Sarungi (28) walifika nyumbani kwa Beatha ili kufanya fumanizi ambapo walifunga kwa nje mlango wa kuingilia kwa kufuli ili kumzuia mgoni wake na mkewe, Beatha wasiweze kutoka wakati wakienda kutoa taarifa kwa uongozi wa Serikali ya Kijiji hicho.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa Lingston na Beatha wakiwa ndani ya nyumba hiyo usiku huo walisikia mlango wa kutokea nje ukifungwa kwa kufuli hivyo waliamua kuuvunja ili waweze kutoka ndipo Lingston na mdogo wake alipoaghairi kwenda kutoa taarifa kwa uongozi wa Serikali ya kijiji hicho na kuanza kuushikilia mlango huo ili 'watuhumiwa' wao wasiweze kutoka na kukimbia.
Hata hivyo, kwa mujibu wa Mwendesha Mashitaka, Lingston na Beatha waliwazidi nguvu Richard na mdogo wake na kuweza kuuvunja mlango huo.
Ndipo Lingston na Beatha walipoanza kuwashambulia Richard na mdogo wake kwa panga na msumeno ambapo kufuatia maumivu waliyoyapata kwa kipigo hicho walipiga mayowe ya kuomba msaada ambapo majirani walifika nyumbani hapo na kuwakamata washtakiwa hao wawili.
Chanzo;Habari Leo
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa