Mwenyekiti
wa Tasisi ya REYO Abdallah Rubega (Flana Nyeupe) akitoa maelezo juu ya
aina ya miti itakayopandwa katika msitu wa Wangabo kwa heshima ya Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo
Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akiwa katika picha ya pamoja na
wadau wa mazingira huku ameshikilia bango la kuhamasisha wananchi kuacha
kuchoma moto misitu na kuendelea kutunza vyanzo vya maji.
Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akipanda mti ishara ya kufungua
upandaji miti Mkoani Rukwa iuli kufikia lengo la mkoa la kupanda miti
milioni 6, Maadhimisho yaliyofanyika katika Shule ya Sekondari Matai,
Wilayani kalambo.
Mkuu
wa Wilaya ya Sumbawanga Dk. Khalfan Haule (kulia) akisaidiana na baadhi
ya wananfunzi wa Shule ya Sekondari Matai kupanda miti ikiwa ni juhudi
za kuwaelimisha wananfunzi umuhimu wa kupanda miti.
Mmoja
wa Wananfunzi wa Shule ya Sekondari Matai, Joseph Katepa akiwa amepumua
baada ya kupanda miti kadhaa katika eneo lililoandaliwa maalum kwa
kupanda miti katika shule hiyo.
Wanafunzi mbalimbali wakiendelea kupanda miti katika eneo lililoandaliwa maalum kwa kupanda miti katika shule hiyo.
Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ameziagiza Halmashauri nne za Mkoa
wa Rukwa kuhakikisha zinafikia lengo la kupanda miti milioni 1.5 kila
moja hadi kufikia mwisho wa mwaka wa 2017/2018 ili kufikia lengo la Mkoa
la kupanda miti milioni 6 katika kutekeleza sera ya kupanda miti
kitaifa.
Amesema
kuwa Halmashauri itakayoshindwa kufikia lengo itatakiwa kulipa faini ya
shilingi Milioni 1 kuilipa Halmashauri itakayofika lengo ambapo
Halmashauri Mshindi inategemewa kupata shilingi Milioni 3 na fedha hizo
itapewa taasisi itakayopanda miti mingi kuliko taasisi nyingine ya
serikali ndani ya Halmashauri iliyoshinda hasa mashule ili kuwafundisha
wanafunzi umuhimu wa kupanda miti.
“Halmashauri
ambayo haikufikia lengo imuume kutoa shilingi Milioni 1 kumlipa
mwenzake, katika hizo Halmashauri 4, kwa maana mshindi atapata shilingi
Milioni 3, lakini endapo Halmashauri zote zitafikia malengo nitazipa
Halmashauri Shilingi Milioni 1, na hiyo fedha itakwenda kwenye taasisi
iliyopanda miti mingi kuliko taasisi nyingine hasa mashule,” Mh. Wangabo
alibainisha.
Ameongeza
kuwa mwaka ujao wa 2018/2019 halmashauri itakayoshindwa kufikia lengo
la kupanda miti Milioni 1.5 italipa faini ya shilingi Milioni 5 ili kila
halmashauri iweze kufikia lengo na kutimiza maelekezo ya serikali na
kuwaonya wote wenye tabia ya kuchoma misitu jambo linalokwamisha
jitihada za kutunza mazingira.
Ameyasema
hayo alipokuwa akizindua wiki ya kupanda miti Kimkoa iliyofanyika
katika katika Shule ya Sekondari Matai, Wilaya ya kalambo ambapo miti
100 ilipandwa katika uwanja uliopewa jina la Msitu wa Wangabo kama
kuunga mkono juhudi za Mh. Joachim Wangabo katika kuhakikisha kuwa Mkoa
wa Rukwa haubaki kuwa jangwa hasa kwa kilimo kinachotegemea mvua.
Nae
akisoma risala Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Mh. Julieth Binyura kabla ya
kumkaribisha Mh. Wangabo alisema kuwa miongoni mwa mikakakti iliyowekwa
na Wilaya hiyo ni kuhakikisha kila Kaya inapanda miti mitano na
kuhakikisha kila shule inatenga eneo la kupanda miti ya matunda na mbao.
Pia
alitumia nafasi hiyo kutoa takwimu za miti iliyopandwa na Wilaya hiyo,
“kwa mwaka 2016/2017 miti 497,896 ilipandwa na kwa mwaka 2017/2018
mategemeo ya Wilaya ni kupanda miti Milioni 1.5 pamoja na changamoto za
mifugo pamoja na wananchi kukosa hamasa ya kupanda miti tutahakikisha
tunatoa elimu na kutenga bajeti kwaajili ya shughuli hiyo,” Alisema.
Kwa
upande wake Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dk. Khalfan Haule amesema kuwa
mkakati wa Wilaya ni kuhakikisha kila mwanafunzi kwa shule za msingi na
sekondari anapatiwa mti na uongozi wa shule autunze na ukivunwa
asilimia 40 atapewa mwanafunzi na asilimia 60 itabaki shuleni.
Nazo
taasisi mbalimbali za utunzaji wa mazingira wameahidi kushirikiana na
Halmashauri katika kutoa elimu na kuwa na vijiji vya mfano ambavyo
wanakijiji wanaweza kutoa ushuhuda juu ya elimu ya mti waliyoipata na
faida mabazo zimepatikana kutokana na wingi wa miti watakayokuwa nayo
katika vijiji.
Kwa
mwaka 2016/2017 Mkoa wa Rukwa ulipanda miti 2,489,296 ambayo ni sawa na
asilimia 41.5 ya lengo na mwaka 2017/2018 hadi sasa Mkoa umepanda miti
2,173,649 ambayo ni sawa na asilimia 36.22.
0 comments:
Post a Comment