Imeandikwa na Peti Siyame, Sumbawanga
WATU watano wakiwemo watoto wawili wamekufa katika matukio tofauti
yaliyotokea mkoani hapa hivi karibuni ambapo mganga wa jadi, Levocatus
Kanjalanga (65) aliuawa kikatili kwa kuchomwa mkuki mgongoni na mtu
asiyefahamika.
Matukio hayo ambayo yametokea katika Wilaya za Nkasi, Kalambo na
Manispaa ya Sumbawanga yamethibitishwa kwa nyakati tofauti na Kamanda wa
Polisi wa Mkoa wa Rukwa, George Kyando (pichani) na Mkuu wa Wilaya ya
Nkasi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya,
Said Mtanda.
Mtoto wa mganga huyo, Simon Kanjalanga alilieleza gazeti hili kuwa
baba yake aliuawa juzi saa moja na nusu asubuhi kwa kupigwa na mkuki
mgongoni akiwa anatembea mitaani katika kitongoji cha Chawe kilichopo
katika Mji wa Namanyere wilayani Nkasi.
Taarifa kutoka eneo hilo la tukio zinaeleza kuwa mganga huyo wa
kienyeji alikuwa akituhumiwa na wateja wake kuwa alikuwa akiwatoza fedha
nyingi za matibabu lakini walikuwa hawaponi kupitia uganga wake huo.
Akithibitisha Mkuu wa Wilaya hiyo, Mtanda alieleza kuwa watu wawili
wameuawa kikatili wilayani humo akiwemo mganga huyo kwa kile
kinachodaiwa kuwa ni imani za kishirikina .
CHANZO HABARI LEO
0 comments:
Post a Comment