Na. Immaculate Makilika- MAELEZO
Udhibiti
wa huduma ya habari kwa namna ya ili kulinda usalama, utulivu amani
na maslahi ya kiuchumi, maadili au afya ya jamii ni jambo jema ambalo
huzingatiwa na nchi zote duniani.
Hayo
yamesemwa na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Diplomasia, Dkt. Bernard Achiula
alipokuwa akifanya mahojiano kuhusu namna muswada sheria ya huduma za
habari unavyoweza kusaidia kukuza diplomasia ya uchumi nchini.
Dkt.
Achiula alisema kuwa vyombo vya habari vina jukumu kubwa la kulinda
amani ya nchi na kwa kuwekwa misingi ya uwajibikaji kwa waandishi wa
habari itakayosaidia kulinda maslahi ya Taifa.
“Muswada
huu upitishwe ili vyombo vya habari vifanyekazi katika misingi ya
taaluma kwa kutoa taarifa zenye kweli kwa jamii, zitakazoitangaza nchi
kimataifa ili kujenga diplomasia ya uchumi, itakayosaidia katika
kulinda heshima utulivu na amani ya nchi”
“Muswada
huu pia utasaidia waandishi wa habari kuandika habari zitakazoiletea
sifa nchi na kuvutia watalii na wawekezaji kwa kuzingatia amani iliyopo
nchini, mbali na hapo diplomasia ya uchumi itaweka mazingira rafiki
katika kufikia azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Tanzania ya kufikia
uchumi wa kati kupitia viwanda ifikapo mwaka 2020” alisema Dkt. Achiula
Sehemu
hii ya muswada wa huduma za habari unaakisi mikataba ya kimataifa
ikiwemo mkataba wa geneva ibara ya 19 inayoainisha haki wa wajibu kwa
mwandishi wa habari hasa katika maeneo yanayohusu usalama, utulivu amani
na maslahi ya kiuchumi, maadili au afya ya jamii.
Akizungumzia
kuhusu Bodi ya Ithibati iliyopo katika muswada huo, Dkt. Achiula
alisema kuwa Bodi hiyo itasaidia kukuza kanuni za maadili kwa wanahabari
na kukuza weledi jambo litachochea mahusiano yenye faida katika nyanja
za kimataifa.
Ameongeza
kuwa kuwemo kwa Baraza Huru la Habari kutasaidia kuijengea uwezo
sekta habari nchini kwa vile muswada huo utazalisha waandishi wa
habari waliobobea katika fani mbalimbali, huku akitolea mfano nchi
zilizoendelea ikiwemo Ujerumani kwa kuwa na chombo kinachosimamia
masuala ya sekta ya habari kwa kufuata misingi na utaratibu maalumu.
Aidha,
wadau wa sekta ya habari nchini, wametakiwa kuendelea kutoa maoni yao
ya kuboresha Muswada wa huduma za habari, kabla muswada huo kusomwa
tena bungeni ifikapo novemba mosi, mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment