Home » » Madiwani Kalambo waridhia uanzishwaji CHF

Madiwani Kalambo waridhia uanzishwaji CHF

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo, mkoani Rukwa, limeridhia kupitisha sheria itakayoruhusu kuanzishwa kwa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).
Wakipitisha sheria hiyo ndogo, wajumbe wa baraza hilo walisema walikuwa wakisubiri kwa hamu kupelekwa kwa mswada huo ambao utawasaidia wapiga kura wao kuondokana na adha ya kupata matibabu pindi wanapougua na hawana hela za matibabu.
Diwani wa Kisumba, Paul Kasitu, alisema kutokana na kupitishwa sheria hiyo, wananchi wa Kalambo watakuwa na uhakika wa kutibiwa hata kama hawana hela.
Alisema wakazi hao wamekuwa wakipata shida pindi wanapougua, na hasa ikizingatiwa wananchi wengi hawana utaratibu wa kuweka akiba ya hela katika taasisi za kifedha.
Diwani wa Viti Maalumu, Crisensia Nyembela, alisema kuanzishwa kwa mfuko huo kutasaidia wajawazito na watoto ambao ndio wanakuwa waathirika wakubwa, kwani ni kundi ambalo linahitaji huduma za afya kwa umakini wa hali ya juu.
Chanzo:Mwananchi
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa