Home » » ‘Serikali yazuia halmashauri’

‘Serikali yazuia halmashauri’

SERIKALI kupitia wakala wake wa kununua na kuhifadhi mazao ya chakula nchini (SGR), imezitikisa halmashauri nne za Mkoa wa Rukwa baada ya kushindwa kuzilipa zaidi ya sh bilioni 2 za mahindi yaliyonunuliwa.
Kilio cha halmashauri hizo kimetolewa juzi na wajumbe wa Jumuiya ya Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT) Mkoa wa Rukwa kutokana na hatua ya Mkuu wa Wilaya  ya Nkasi, Iddy Kimanta, alipozitupia lawama halmashauri hizo kwamba zina ulegevu katika ukusanyaji wa mapato.
Kutokana  na kauli hiyo, wajumbe wa ALAT wameitaka serikali kupitia SGR/ NFRA kuzilipa halmashauri zote fedha wanazozidai kwa kuwa huko ni kuchelewesha utoaji wa huduma za kijamii kwa muda unaotakiwa.
Mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Rukwa, Godfrey Schona, alisema halmashauri za Mkoa wa Rukwa nyingi zinategemea mapato ya ndani kupitia ushuru wa mazao ya mahindi kiasi cha kupanga mipango mbalimbali ya maendeleo na moja kati ya fedha hizo ni za makusanyo ya ushuru wa mahindi, hivyo serikali inavyoshindwa kupeleka fedha hizo kwa wakati ni kuziua.
Alisema taarifa za serikali zinaonyesha Mkoa wa Rukwa ni wa mwisho katika ukusanyaji wa mapato ya ndani na kuwa moja kati ya vitu vinavyochangia mapato kushuka ni serikali kushindwa kuzipatia halmashauri fedha zake za ushuru wa mahindi kwa wakati.
Mmoja wa wajumbe wa kikao hicho na ambaye pia ni Meya wa Manispaa ya Sumbawanga, Sebastian Katepa, alisema ni mambo ya kushangaza kuona kuwa serikali imekuwa ikisisitiza suala la makusanyo ya ndani kwa halmashauri wakati yenyewe kupitia wakala wake wa SGR/NFRA inashindwa kuzilipa ushuru uliowekwa kwa mujibu wa sheria ndogondogo.
Awali akifungua kikao hicho, mkuu huyo wa wilaya alisema suala la makusanyo ya mapato ya ndani, ni muhimu na kuwa kushuka kwa mapato hayo kutaziua halmashauri husika, jambo ambalo halipaswi kufikiwa.
Chanzo;tanzania daima
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa