Home » » Mvua yaleta maafa

Mvua yaleta maafa

Sumbawanga. Mvua kubwa iliyonyesha juzi katika Kijiji cha Kasense, imesababisha hasara ya Sh88 milioni, baada ya kuharibu nyumba mbalimbali zikiwamo za wanakijiji, taasisi na nyumba za ibada, likiwapo Kanisa Katoliki.
Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa, Kassimu Sengusa alisema hayo jana wakati akizungumza na gazeti hili aliyetaka kujua tathmini ya hasara iliyowapata wananchi baada ya mvua hiyo kunyesha.
Kaimu Mkurugenzi huyo alisema baada ya timu ya wataalamu wa manispaa hiyo kufika eneo la tukio na kufanya tathmini walibaini hasara iliyopatikana ni Sh88 milioni, na kwamba nvua hiyo iliyoambatana na upepo mkali iling’oa paa za nyumba za watu 28, na nyumba mbili za waganga wa zahanati ya kijiji hicho.
Chanzo;Mwananchi
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa