Home » » ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM,NDUGU KINANA YAKUMBANA NA CHANGAMOTO ZA BARABARA WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM,NDUGU KINANA YAKUMBANA NA CHANGAMOTO ZA BARABARA WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akimueleza jambo Mbunge wa jimbo la Nkasi Kaskazini,Mh.Ali Mohammed Kessy,walipokuwa wakitembea kwa miguu kufuatia msafara huo kukumbana na changamoto ya barabara mapema jana jioni katikati ya Msitu wa hifadhi ya wilaya ya Nkasi.Ndugu Kinana na Msafara wake ulikuwa umetoka kijiji cha Namanyere kuelekea kijiji cha Mwampemba kusikiliza matatizo ya Wananchi na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopangwa kutekelezwa kwenye Ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010.

Barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 100,lakini iliwachukua zaidi ya masaa 12 kwenda na kurudi kutokana na ubovu wa barabara.Ndugu Kinana yuko Mkoani Rukwa,Katavi na Kigoma kwa ziara ya siku 21 ya kuimarisha Chama cha CCM,kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo kiwemo na kuzisikiliza kero mbalimbali za wananchi
 Ndugu Kinana akishiriki kuweka mawe sehemu korofi,angalau kusaidia Lori hilo pichani lililolala ndani ya msitu huo kwa siku mbili,wapite nae msafara wake uweze kuendelea na safari.
 Sehemu korofi ya Barabara ikiwekwa sawa ili lori lipite na kisha msafara nao uweze kupita,lakini hata hivyo zilitumika juhudi kubwa kuvusha msafara wa Kinana na hatimae kuendelea na safari ya kuelekea kijiji kingine.
 Ndugu Kinana akizungumza na baadhi ya Wanahabari aliokuwa ameambatana nao kwenye msafara wake,baada ya magari kunasa kutokana tatizo la barabara
 Wanahabari waliokuwa kwenye msafara wa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana wakiwa hoi kabisa,wakisubiri kudra za Mwenyezi Mungu,msafara wa magari yao yanasuliwe na kuendelea na safari.Picha hii imepigwa na Katibu Mkuu,Ndugu Kinana.
 Hali ilikuwa tete mnoo,kipande cha kilometa mia kinapitika kwa zaidi ya masaa sita,kutoka kijiji kimoja kwenda kingine.
 Ilikuwa ni shughuli nzito katika msafara wa Ndugu Kinana,barabara ni mbovu kupita maelezo
 Kila mmoja akipumua kivyake,baada ya kuvuka salama sehemu korofi ya barabara.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana (alinaerusha jiwe) akishiriki kuziba sehemu korofi kwa mawe,ili msafara uweze kupita
 Pichani kulia ni Katibu Mkuu wa CCM,Ndug Kinana akiongoza kuvuka sehemu korofi ya barabara kwa miguu,huku madera wakipiga hesabu zao namna ya kupita.
Mchuma ukipita sehemu korofi ya barabara kwa mbinde.PICHA NA MICHUZIJR-MICHUZI MEDIA GROUP-NKASI RUKWA.
SIKILIZA TONE RADIO HAPA

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Rukwa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa